Page 38 - Historia_Maadili
P. 38
maarufu. Hata hivyo, mavazi ya kitamaduni yaliendelea kutumika, hasa katika maeneo
ya vijijini na miongoni mwa wale waliopinga ushawishi wa wakoloni na tamaduni
za Ulaya Magharibi.
Aidha, maadili ya Kitanzania wakati wa kuingia kwa ukoloni yalikuwa na nguvu
kubwa katika maisha ya watu na yalidumishwa kwa umakini na viongozi wa jadi
FOR ONLINE READING ONLY
pamoja na wazee wa mila. Kanuni hizi za kimaadili zilifanya kazi kama misingi
imara iliyojenga jamii. Jamii pia ilionesha uwajibikaji mkubwa katika kutekeleza
wajibu wao kwa familia na jamii kwa ujumla. Maadili haya yaliziwezesha jamii za
Kitanzania kujiendeleza na kusaidia kuunda jamii zenye utulivu, mshikamano na
maendeleo endelevu.
Kazi ya kufanya 2.3
Tafuta taarifa kutoka vyanzo mbalimbali ikiwemo mtandao na eleza jinsi mavazi
yanaweza kutumika katika kudumisha maadili ya Kitanzania.
Zoezi la 2.2
1. Ainisha maadili yanayopaswa kudumishwa katika jamii yako.
2. Pendekeza mikakati ya kudumisha maadili katika jamii yako.
3. Eleza jinsi teknolojia inavyoathiri maadili katika jamii unayoishi.
4. Ni kwa namna gani hadithi na masimulizi yanaweza kutumika katika
kujenga uzalendo katika mazingira ya sasa.
5. Eleza umuhimu wa lugha za asili katika kudumisha maadili katika mazingira
ya sasa.
Athari za mfumo wa ukoloni katika maadili ya Kitanzania
Kuingia kwa mfumo wa kikoloni katika jamii za Kitanzania kuliathiri mifumo ya
maadili ya kijamii, kiutamaduni, kisiasa na kiuchumi. Athari hizi zinaelezwa kwa
upana katika sehemu zinazofuata.
Athari za kijamii
Elimu: Kabla ya ukoloni, elimu katika jamii za Kitanzania ilitolewa kulingana na
mazingira yao na ilijikita katika mila na desturi. Kulikuwa na mfumo rasmi wa
30
03/10/2024 18:15:10
HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd 30
HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd 30 03/10/2024 18:15:10

