Page 36 - Historia_Maadili
P. 36

hizo, wanajamii waliweza kujenga uzalendo, ujasiri, upendo, fahari na mshikamano
          wa kijamii.

          Simulizi na hadithi: Simulizi na hadithi zilikuwa nguzo muhimu za mawasiliano
          katika jamii za Kitanzania. Kila jamii ilikuwa na aina zake za masimulizi yaliyoakisi
          tamaduni zao. Baadhi ya masimulizi hayo ni kama vile hekaya, methali, vitendawili na
        FOR ONLINE READING ONLY
          hadithi, ambazo zilitumika kufundisha, kuendeleza na kurithisha  maadili ya kitamaduni

          kutoka kizazi kimoja hadi kingine. Kwa mfano, hadithi zilikuwa na masimulizi ya
          matukio mbalimbali ya kijamii yaliyotokea katika vipindi vya nyuma ndani ya jamii
          husika. Hivyo, hadithi hizi ziliwafundisha, ziliwaburudisha na kuwaonya na kwa njia
          hiyo ziliweza kusaidia katika ujenzi wa maadili ndani ya jamii. Mathalani, jamii ya
          Wahehe ilitumia ushairi kama njia ya kuwasilisha ujumbe, kuwaelimisha vijana na
          kuwaburudisha. Simulizi hizi zilikuwa muhimu sana katika kuudumisha utambulisho
          wa kitamaduni na maadili ya kijamii. Wazee wa jamii walikuwa wahusika wakuu

          katika utoaji wa simulizi na hadithi hizi.



           Kazi ya kufanya 2.2


            Tafuta taarifa kutoka vyanzo mbalimbali ikiwemo mitandao kuhusu lugha ya
            kabila mojawapo la Tanzania. Kisha, bainisha misemo au methali au vitendawili
            vya makabila hayo ambavyo vinalenga kudumisha maadili ya Kitanzania.



          Mavazi: Wakati wa kuingia kwa ukoloni, jamii za Kitanzania zilikuwa na mavazi ya
          asili yaliyotengenezwa kwa kutumia malighafi za kiasili kama vile ngozi za wanyama,
          majani na magome ya miti. Vilevile, walivaa mapambo kama hereni na bangili.
          Mavazi haya yalikuwa sehemu ya utambulisho na yaliheshimu utamaduni wa kabila
          au jamii iliyohusika. Vitu hivyo vilikuwa zaidi ya mavazi kwani viliashiria umuhimu
          wa utamaduni uliowakilisha, hadhi, umri na hali ya ndoa ndani ya jamii.

          Vilevile, jamii za Wachaga wanaoishi kwenye miteremko ya Mlima Kilimanjaro
          walikuwa wakivaa mavazi yaliyotengenezwa kwa ngozi ya wanyama au vitambaa
          vilivyofumwa kienyeji. Mavazi haya mara nyingi yalikuwa rahisi na yalifaa kwa hali
          ya hewa ya mlima. Hata hivyo, baada ya kuwasili kwa ukoloni, mavazi ya mtindo
          wa Kimagharibi yalianza kuathiri mavazi yao, hasa miongoni mwa vijana na wale
          waliojihusisha na biashara au shughuli za kimisionari. Hii ilikuwa ni sehemu ya
          harakati za wazungu kutafuta masoko kwa bidhaa za viwanda vyao vya Ulaya.





                                                  28




                                                                                        03/10/2024   18:15:10
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   28
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   28                                         03/10/2024   18:15:10
   31   32   33   34   35   36   37   38   39   40   41