Page 31 - Historia_Maadili
P. 31

Sura ya Pili                   Athari za ukoloni katika

                                                 maadili ya Kitanzania


        FOR ONLINE READING ONLY



                   Utangulizi



            Kuingia kwa ukoloni mwishoni mwa karne ya 19 kulisababisha kuanza
            kupenya kwa maadili ya kikoloni, ambayo yaliidhoofisha mifumo asilia ya
            maadili ya jamii za Kitanzania. Katika sura hii, utajifunza kuhusu dhana ya
            maadili katika kipindi cha ukoloni na maadili ya jamii za Kitanzania wakati
            wa kuingia kwa ukoloni. Vilevile, utajifunza athari za mfumo wa ukoloni
            katika maadili ya Kitanzania na maadili ya Kitanzania yaliyodumishwa
            katika kipindi cha ukoloni. Umahiri utakaoujenga utakuwezesha kuishi kwa
            kuzingatia maadili ya Kitanzania.






                   Fikiri



             Maadili ya sasa ya jamii za Kitanzania.



          Dhana ya maadili wakati wa ukoloni

          Dhana ya maadili wakati wa ukoloni inahusisha mifumo ya kiutawala, kisiasa,
          kiuchumi na kiutamaduni ambayo ililetwa na wakoloni pamoja na ile iliyokuwepo
          kabla ya ujio wa wakoloni katika jamii za Kitanzania. Kwa kiasi kikubwa, Waafrika
          waliendelea kuziishi na kuzifuata mila na desturi zao, ingawa pia waliyapokea maadili
          mapya kama vile imani za kiroho, mifumo ya kiutawala na tamaduni za kigeni. Kanuni
          za kikoloni zilisisitiza uwajibikaji wa kila mtu, umiliki binafsi wa mali na heshima
          kulingana na nafasi ya mtu katika jamii. Hata hivyo, kanuni hizi kwa kiasi kikubwa
          zilikinzana na maadili ya Kitanzania yaliyokuwapo kabla ya ujio wa wakoloni.
          Hii ni kwa sababu jamii nyingi ziliamini katika uwajibikaji wa pamoja, umiliki wa
          mali kwa pamoja na heshima kwa wote bila kujali nafasi ya mtu katika jamii. Kwa
          ujumla, maadili ya jamii za Kitanzania kabla ya ujio wa ukoloni katika jamii nyingi
          yaliongozwa na mfumo wa usawa.

                                                  23




                                                                                        03/10/2024   18:15:09
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   23
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   23                                         03/10/2024   18:15:09
   26   27   28   29   30   31   32   33   34   35   36