Page 29 - Historia_Maadili
P. 29

kahawa na yale maeneo waliyotokea manamba. Hivyo, miundombinu hiyo wakati
          wa utawala wa Waingereza ilisaidia katika kuwasafirisha manamba kwenda kufanya
          kazi kwenye mashamba na migodi. Pia, miundombinu ya barabara na reli ilitumika
          kusafirisha malighafi kutoka bara hadi bandarini, kusambaza bidhaa za viwandani
          kutoka bandarini hadi bara. Vilevile, kusafirisha askari kwenda maeneo yaliyokuwa
          na upinzani na hatimaye, kusafirisha watawala kwenda kusimamia shughuli katika
        FOR ONLINE READING ONLY
          maeneo mbalimbali. Huduma za usafirishaji wakati wa utawala wa Waingereza
          hazikulenga moja kwa moja kuwanufaisha Waafrika kama abiria, bali zililenga
          kurahisisha mipango na matakwa ya kikoloni ya unyonyaji na ukandamizaji wa
          wananchi, pamoja na kusafirisha malighafi kwenda Ulaya kwa ajili ya viwanda vyao.

          Huduma za maji na umeme: Serikali ya Uingereza ilijitahidi kuwapa wananchi wa
          Tanganyika na Zanzibar huduma za maji na umeme ili kuwawezesha kuwa na afya
          bora ili kuendelea kuzalisha malighafi. Baada ya Vita Kuu ya Pili ya Dunia, serikali
          ilipanua huduma hizi, upanuzi ambao ulifanyika zaidi katika maeneo ya mijini na
          ya uzalishaji. Maeneo hayo ni kama vile mashamba ya kikoloni, migodini na mahali
          walipoishi watawala wa kikoloni.

          Ubaguzi wa rangi ulijitokeza katika utoaji wa huduma za maji na umeme. Ubaguzi
          huu ulidhihirika zaidi katika maeneo ya mijini. Huko huduma bora za maji na umeme
          walipatiwa kwanza Wazungu, wakifuatiwa na Waasia na hatimaye Waafrika. Kutokana
          na hali hii, baadhi ya maeneo ya miji mikubwa kama Dar es Salaam na Mwanza
          yalijulikana kama Uzunguni na Uhindini. Maeneo ya mjini walipokaa Waafrika
          wengi yaliitwa maeneo ya Uswahilini. Maeneo ya vijijini yalipatiwa huduma duni
          zaidi ikilinganishwa na yale ya mijini, hali iliyosababisha watu wa vijijini kuhangaika
          kutafuta huduma za maji na umeme. Maeneo ya vijijini yaliendelea kutumia kuni,
          koroboi na taa za chemli kutoa mwanga wakati wa usiku.

          Mchango wa ukoloni katika uhusiano wa Tanzania na mataifa yaliyoitawala
          Kabla ya ujio wa wakoloni, jamii za Kitanzania zilikuwa na uhusiano wa kuheshimiana
          na kushirikiana na jamii nyingine za Afrika na kwingineko. Uhusiano huu ulijengwa
          kwa misingi ya biashara, ambapo jamii hizo zilibadilishana bidhaa kama vile dhahabu,
          pembe za ndovu na vyakula. Ushirikiano huu ulizingatia maadili ya kutegemeana,
          kusaidiana na kuaminiana. Biashara iliyofanyika kati ya jamii hizi ilichangia
          kuchochea maendeleo ya kijamii na kiuchumi.

          Hali hii ya ushirikiano ilianza kubadilika baada ya ujio wa wakoloni kutoka Ulaya
          Magharibi. Mataifa ya Ulaya, hususani Ujerumani na Uingereza, yalitawala maeneo
          mbalimbali kwa lengo la kunyonya rasilimali za jamii za Kitanzania. Wakoloni
          walivunja uhusiano wa asili uliokuwepo kwa kuanzisha mipaka mipya na kuleta
          maadili ya kikoloni. Pia, waliweka sera mpya zilizovuruga maadili ya kijamii ya
          Kitanzania, ambayo yalijengwa katika misingi ya utu, upendo, umoja, kusaidiana
          na kuheshimiana kama jamii huru.

          Baada ya ukoloni kushamiri, uhusiano kati ya jamii za Kitanzania na wakoloni uliingia
          katika hali ya uhasama mkubwa. Mataifa ya kikoloni ya Ulaya Magharibi yalitumia

                                                  21




                                                                                        03/10/2024   18:15:09
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   21                                         03/10/2024   18:15:09
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   21
   24   25   26   27   28   29   30   31   32   33   34