Page 28 - Historia_Maadili
P. 28

ambapo kulikuwa na hospitali maalumu kwa Wazungu na nyingine kwa ajili ya watu
          wenye rangi nyingine. Kwa mfano, Hospitali ya Ocean Road ilikuwa maalumu kwa
          Wazungu, kwa kuwa ilitoa huduma bora zaidi.


          Miundombinu: Katika kutekeleza mpango wa ukoloni wa kupata malighafi muhimu
          kwa ajili ya viwanda vya Ulaya, Waingereza waliendelea kufufua na kuanzisha
        FOR ONLINE READING ONLY
          miundombinu kutoka maeneo ya pwani hadi maeneo ya uzalishaji mali kama migodi
          na mashamba ya pamba, mkonge na kahawa. Miundombinu iliyojengwa ni pamoja
          na barabara, reli na bandari. Reli kutoka Tabora hadi Mwanza ilikamilishwa mwaka
          1928. Pia, usafiri katika Ziwa Tanganyika na Viktoria uliimarishwa. Bandari za Tanga
          na Dar es Salaam, ambazo zilikuwa zimeathiriwa na vita, zilikarabatiwa. Waingereza
          pia walijenga bandari ya Mtwara. Aidha, miundombinu mingine ya reli iliongezwa
          kwa lengo la kusafirisha malighafi na vibarua kutoka sehemu mbalimbali za nchi,
          kama inavyoonekana kwenye Kielelezo 1.5.
















































                     Kielelezo 1.5: Miundombinu ya reli wakati wa utawala wa Waingereza
          Miundombinu ya barabara, reli na usafiri wa majini ililenga kuunganisha maeneo
          muhimu ya uzalishaji mali, kama vile mashamba ya mkonge, pamba, karanga na
                                                  20




                                                                                        03/10/2024   18:15:09
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   20
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   20                                         03/10/2024   18:15:09
   23   24   25   26   27   28   29   30   31   32   33