Page 23 - Historia_Maadili
P. 23

Zoezi la          1.4

           1.  Fafanua namna mabadiliko katika mfumo wa utawala wa jadi kufuatia kuja
                kwa Wajerumani yalivyoathiri jamii za Kitanzania.
           2.  Kwa nini jamii za Kitanzania zilipinga ulipaji wa kodi ulioanzishwa na
        FOR ONLINE READING ONLY
                utawala wa Kijerumani?

           3.  Unajifunza nini kutoka kwa mababu na mabibi zetu waliopinga mfumo na
                utawala wa Kijerumani?


          Utawala wa Waingereza Tanganyika na Zanzibar
          Afrika Mashariki ya Kijerumani ilikuwa sehemu ya koloni la Ujerumani hadi
          kumalizika kwa Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia mwaka 1918. Wakati wa vita hivyo,
          koloni la hili lilitekwa na majeshi ya Uingereza na Ubelgiji. Mkataba wa Amani
          wa Versailles wa mwaka 1919 uliamua kwamba makoloni yote yaliyokuwa ya
          Wajerumani yakabidhiwe mataifa yaliyoshinda vita hivyo. Hivyo, Afrika Mashariki
          ya Kijerumani ilikabidhiwa rasmi kwa Waingereza chini ya udhamini wa Jumuiya
          ya Kimataifa (League of Nations).

          Kwa upande wa Zanzibar, utawala wa Waingereza ulianza baada ya kutiwa saini kwa
          mkataba wa pili kati ya Wajerumani na Waingereza. Mkataba huo ulisainiwa  tarehe
          1 Julai, 1890, unaojulikana kama Mkataba wa Heligoland. Kulingana na mkataba
          huo, Uingereza ilipewa mamlaka ya kuiweka Zanzibar chini ya himaya yake kwa
          makubaliano na mtawala wa wakati huo, Sayyid Ali bin Said.

          Jamii za Tanganyika na Zanzibar wakati huo zilifuata mwelekeo wa kiuchumi,
          kisiasa na kijamii ulioanzishwa na Waingereza. Ili kuimarisha ukoloni, Waingereza
          walibadilisha mfumo wa utawala uliokuwapo na kuanzisha mfumo wa kiuwakala
          ambao ulibadilisha pia uchumi, siasa na utamaduni wa Tanganyika. Jambo muhimu
          la kufahamu ni kwamba, ni utawala wa Kiingereza uliobadilisha jina la koloni hilo
          kutoka Afrika Mashariki ya Kijerumani na kuwa Tanganyika.


          Mabadiliko ya kiuchumi wakati wa utawala wa Waingereza

          Mabadiliko ya kiuchumi wakati wa utawala wa Waingereza yalilenga kuendeleza
          kilimo, biashara na viwanda vidogovidogo. Kwa upande wa kilimo, utawala wa
          Waingereza ulihamasisha kilimo cha mazao ya biashara kama vile kahawa, pamba,
          mkonge, chai na pareto. Serikali hiyo pia iliwahimiza walowezi kufufua mazao ya
          biashara ambayo yalikuwa yameathiriwa na vita. Walowezi hawa walitoka mataifa
          mbalimbali kama Uingereza, Afrika Kusini, Ugiriki na India. Lengo kubwa la kufufua
          mazao haya ya biashara lilikuwa kupata malighafi za kutosha kwa ajili ya viwanda
          nchini kwao Uingereza.

                                                  15




                                                                                        03/10/2024   18:15:08
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   15
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   15                                         03/10/2024   18:15:08
   18   19   20   21   22   23   24   25   26   27   28