Page 19 - Historia_Maadili
P. 19

Ujerumani ilichukua rasmi mamlaka ya kutawala Afrika Mashariki ya Kijerumani.
          Wajerumani walikusudia kuimarisha utawala wao katika koloni hili kwa kuzitumia
          mbinu mbalimbali. Mbinu hizo zilijumuisha matumizi ya vyombo vya kiitikadi kama
          vile elimu na dini. Mbinu nyingine ilikuwa ni kuunda vyombo vya dola kama jeshi,
          magereza na mahakama za kikoloni ili kuhakikisha wananchi hawaupingi utawala
          wa kikoloni na wanazitii sheria zilizowekwa. Aidha, walitumia mbinu ya kuwapeleka
        FOR ONLINE READING ONLY
          watawala wazungu katika ngazi za uongozi na kuondoa tawala za jadi. Kwa ujumla,
          ujio wa Wajerumani ulileta mabadiliko makubwa ya kiuchumi, kisiasa na kijamii
          katika jamii za Kitanzania.

          Mabadiliko ya kiuchumi wakati wa utawala wa Wajerumani
          Kama ilivyosemwa awali, lengo kuu la Wajerumani kuja katika Afrika Mashariki ya
          Kijerumani lilikuwa kutafuta suluhisho la changamoto za kiuchumi zilizotokana na
          mapinduzi ya viwanda, kama vile upungufu wa masoko na malighafi, kwa viwanda
          vyao barani Ulaya. Kwa hivyo, kupitia ukoloni, wakoloni waliweza kuzipunguza
          changamoto hizo kwa kuanzisha uchumi wa kikoloni ambao ulileta mabadiliko
          makubwa kwenye jamii za Kitanzania. Shughuli za uzalishaji mali zilitegemea sana
          uzalishaji wa mazao ya biashara kama vile kahawa, chai, mkonge, pamba, tumbaku
          na mpira. Mazao haya yalilimwa katika maeneo mbalimbali ya Afrika Mashariki ya
          Kijerumani. Kwa mfano, kahawa ililimwa Bukoba, Kilimanjaro, Arusha na Tukuyu;
          pamba ilianza kulimwa katika maeneo ya Mwanza, Shinyanga, Morogoro, Bagamoyo,
          Rufiji na Lindi; katani ililimwa huko Tanga, Morogoro, Lushoto, Lindi, Dar es Salaam
          na Pwani; mpira ulilimwa maeneo ya pwani hasa katika bonde la mto Pangani huko
          Tanga na bonde la mto Rufiji hasa maeneo ya  Mohoro. Walowezi wa Kijerumani
          walianzisha mashamba ya katani yenye ukubwa wa ekari zaidi ya 100,000 (hekta
          40,000). Walowezi wengine walipanda zaidi ya miche milioni mbili ya kahawa,
          ekari 200,000 (hekta 81,000) za miti ya mipira na mashamba ya pamba. Maeneo ya
          Rukwa, Kigoma, Mtwara, Dodoma na Singida hayakuruhusiwa kuanzisha kilimo cha
          mashamba makubwa kwa sababu yalitengwa maalumu kwa ajili ya kutoa wafanyakazi
          na vibarua (manamba) watakaofanya kazi katika mashamba makubwa ya walowezi
          na migodi ya madini hasa dhahabu huko Chunya, Sekenke na Mwanza.

          Kwa upande wa viwanda,  Wajerumani hawakuanzisha viwanda vikubwa bali
          walijenga viwanda vidogo, hasa vya kuchakata malighafi ili kupunguza uzito wake
          kabla ya kusafirishwa kwenda Ujerumani.  Kwa mfano, walijenga vinu vya kukoboa
          kahawa, kuchambua pamba na kusindika mkonge. Wajerumani walijenga viwanda
          vidogovidogo vya kuzalisha viatu, viberiti, baruti na risasi. Hivyo, Wajerumani
          hawakujenga viwanda vikubwa vya kuzalisha bidhaa mbalimbali za viwandani kama
          vile nguo, kamba na mazulia, bali walilenga kurahisisha usafirishaji wa malighafi tu.

          Vilevile, Wajerumani waliendesha biashara ya kinyonyaji, kwani koloni hili lilitumika
          kama soko la kuuzia bidhaa za viwandani kutoka Ujerumani, kama vile nguo, baiskeli,


                                                  11




                                                                                        03/10/2024   18:15:07
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   11                                         03/10/2024   18:15:07
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   11
   14   15   16   17   18   19   20   21   22   23   24