Page 21 - Historia_Maadili
P. 21

Afya
          Huduma za afya katika kipindi cha ukoloni zilitolewa kwa ubaguzi wa rangi, ambapo
          huduma hizo zilipatikana katika maeneo ambayo wakoloni walianzisha shughuli
          kubwa za uzalishaji mali kama vile mashamba na makazi yao. Wazawa walipata
          matibabu ya kiwango cha chini ukilinganisha na Wazungu na Waasia. Matibabu haya
          yalilenga kuwawezesha Waafrika kuzalisha malighafi bila kusumbuliwa na magonjwa
        FOR ONLINE READING ONLY
          hasa ya kitropiki au kuumia wakiwa kazini. Aidha, huduma za afya zilitilia mkazo
          matibabu badala ya kinga dhidi ya magonjwa. Madhumuni ya kueneza huduma hizi
          yalikuwa ni kuhakikisha kwamba wazalishaji mali katika maeneo hayo wanakuwa
          na afya njema ili waweze kufanikisha malengo ya kikoloni.

          Athari hasi za huduma hizi zilikuwa ni kupotea kwa umaarufu kwa waganga na
          matabibu wa jadi, pamoja na dawa zao kushuka thamani. Hii ilisababishwa na
          ongezeko la vituo vya matibabu na matumizi ya dawa za kigeni. Hata hivyo,  bado
          waganga wa jadi  waliendelea kutoa matibabu, hasa katika maeneo ya vijijini.

          Huduma za maji na umeme

          Katika kipindi cha ukoloni, huduma za maji na umeme zilitolewa kwa ubaguzi na
          upendeleo, kwani huduma hizi zilielekezwa zaidi katika maeneo yenye umuhimu
          wa kiuchumi. Kwa mfano, usambazaji wa huduma hizi ulifanyika katika migodi,
          viwandani, maeneo ya mijini, mashamba makubwa ya wakoloni na makazi ya
          walowezi wa Kizungu na Kiasia.

          Miundombinu ya mawasiliano
          Wakoloni walijenga njia za uchukuzi na mawasiliano kama vile barabara, reli na
          bandari. Miundombinu hii ilikuwa muhimu kwa usafirishaji wa malighafi, bidhaa
          na watu. Reli na barabara zilijengwa kutoka maeneo ya uzalishaji wa malighafi hadi
          bandarini. Malighafi kutoka makoloni ilisafirishwa  kwenda Ulaya na bidhaa za
          viwandani kutoka Ulaya kama vile nguo, vyombo vya nyumbani na zana za chuma
          ziliingizwa kupitia bandari hizo na kuletwa Afrika Mashariki ya Kijerumani.



           Kazi ya kufanya 1.4
            Kwa kusoma matini katika vitabu na mtandaoni, fanya utafiti mdogo kuhusu
            tiba za jadi wakati wa ujio wa Wajerumani. Utafiti wako ujikite katika maeneo
            yafuatayo:

             (a)  Namna tiba za jadi zilivyokuwa kabla ya ujio wa Wajerumani;
             (b)  Magonjwa yaliyotibiwa kwa kutumia tiba za jadi;

             (c)  Namna Wajerumani walivyoathiri tiba za jadi; na
             (d)  Toa ushauri kuhusu umuhimu wa tiba za jadi kwa jamii  za sasa za
                  Kitanzania.


                                                  13




                                                                                        03/10/2024   18:15:08
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   13                                         03/10/2024   18:15:08
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   13
   16   17   18   19   20   21   22   23   24   25   26