Page 18 - Historia_Maadili
P. 18

ya Kiarabu, huku lugha ya Kiswahili ikiendelea kutumika kama lugha ya biashara
          na mawasiliano ya kila siku.

          Mwingiliano baina ya Waarabu na jamii za pwani ulisababisha mabadiliko makubwa
          ya kitamaduni. Kwa mfano, uvaaji wa mavazi kama vile kanzu, baibui, baraghashia na
          makubadhi ulienea sana. Lugha ya Kiswahili pia ilianza kupata maneno mapya baada
        FOR ONLINE READING ONLY
          ya kutohoa baadhi ya msamiati kutoka lugha ya Kiarabu ili kurahisisha mawasiliano.
          Mfano wa baadhi ya maneno hayo ni kama vile marhaba, shukrani, sheria, heshima,
          nzuri, labeka na hayati. Jamii zilizoathiriwa zaidi na tamaduni za Kiarabu ni pamoja na
          Wahadimu, Watumbatu, Wapemba,Wazaramo na Wakwere kutokana na mwingiliano
          wao wa karibu katika shughuli za kila siku.



           Kazi ya kufanya 1.3

            Soma matini mbalimbali katika vitabu na mtandao kuhusu mabadiliko ya kijamii
            wakati wa utawala wa Waarabu kisha; tengeneza vibonzo vinavyoonyesha namna
            utamaduni, maadili na elimu vilivyobadilika baada ya ujio wa Waarabu.



          Utawala wa Wajerumani
          Utawala wa Wajerumani katika Afrika Mashariki ya Kijerumani ulisukumwa na
          mabadiliko ya kiuchumi yaliyokuwa yakijitokeza barani Ulaya, ikiwemo nchini
          Ujerumani. Mabadiliko hayo yalitokana na kuongezeka kwa teknolojia iliyochochea
          mapinduzi ya viwanda yaliyoshika kasi kuanzia mwaka 1750 nchini Uingereza.
          Mapinduzi hayo yalisababisha uzalishaji mkubwa wa bidhaa na hivyo kuongeza
          mahitaji ya malighafi kwa ajili ya uzalishaji pamoja na masoko mapya na makubwa
          kwa ajili ya kuuza bidhaa hizo. Ili kukabiliana na changamoto hii, Wajerumani, pamoja
          na mataifa mengine ya Ulaya, walitafuta njia za kupata suluhisho kupitia nchi za nje.

          Bara la Afrika lilionekana kuwa eneo muafaka kwa uwekezaji na utatuzi wa
          changamoto za upatikanaji wa malighafi na masoko. Katika robo ya mwisho ya
          karne ya 19, Wajerumani walifika Afrika Mashariki ya Kijerumani baada ya kupata
          taarifa kuhusu uwapo wa malighafi na soko la bidhaa. Taarifa hizo walizipata kutoka
          kwa wamisionari, wafanyabiashara na wapelelezi waliotumwa na makampuni ya
          Kijerumani hapa nchini. Hii iliwasaidia sana kuyatambua maeneo muhimu ya
          kuwekeza  na  kuanzisha  mashamba  makubwa  ili  kupata  malighafi  mbalimbali
          zilizohitajika katika  viwanda vya Ujerumani.
          Utawala wa Wajerumani katika eneo hili unaweza kugawanywa katika vipindi
          vifuatavyo: Kati ya mwaka 1886 hadi 1891. Kipindi hiki, Afrika Mashariki ya
          Kijerumani ilitawaliwa na Kampuni ya Kijerumani ya Afrika Mashariki chini ya
          uongozi wa mfanyabiashara Karl Peters. Kuanzia mwaka 1891 hadi 1918, serikali ya


                                                  10




                                                                                        03/10/2024   18:15:07
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   10
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   10                                         03/10/2024   18:15:07
   13   14   15   16   17   18   19   20   21   22   23