Page 20 - Historia_Maadili
P. 20

mapanga, majembe, viatu na sigara. Bidhaa hizi zote ziliuzwa kwa bei kubwa, wakati
          malighafi zilizotumika kuzalisha bidhaa hizo zilinunuliwa kwa bei ndogo sana.


                              Zoezi la          1.3


        FOR ONLINE READING ONLY
           1.  Fafanua sababu zilizowafanya Wajerumani kuanzisha utawala wa kikoloni
               katika jamii za Kitanzania.

           2.  Kwa nini Wajerumani walijenga viwanda vidogo badala ya viwanda vikubwa
               katika Afrika Mashariki ya Kijerumani?

           3.  Eleza  athari ambazo  zingetokea  iwapo  Wajerumani wangejenga  viwanda
               vikubwa vya kuchakata malighafi katika Afrika Mashariki ya Kijerumani.



          Mabadiliko ya kijamii wakati wa utawala wa Wajerumani
          Wajerumani walilazimika kujenga na kutoa huduma kadhaa ili kufanikisha malengo
          yao katika Afrika Mashariki ya Kijerumani. Huduma hizi zilijumuisha elimu, afya,
          maji na umeme, pamoja na miundombinu ya mawasiliano.

          Elimu

          Elimu iliyotolewa na Wajerumani ililenga kukidhi mahitaji ya shughuli zao za
          kikoloni. Mfumo wa elimu uliundwa mahususi ili kuandaa wasaidizi watakaowasaidia
          Wajerumani katika shughuli hizo. Elimu hiyo ililenga zaidi wananchi wachache
          ambao wangeweza kuzalisha malighafi kwa ajili ya kukidhi mahitaji ya uchumi wa
          kikoloni. Malengo ya elimu hiyo yalikuwa yafuatayo:

           (a)  Kueneza utamaduni wa Kijerumani;
           (b)  Kuandaa watumishi wa ngazi za chini;

           (c)  Kufundisha uadilifu  na maadili ya kazi; na

           (d)  Kuandaa wazalishaji mali kwa ajili ya uchumi wa Kijerumani.

          Ili kutimiza malengo hayo, mtaala wa elimu ya Kijerumani ulifundisha stadi kama
          vile uashi, useremala, ukarani, upigaji picha, ufundi wa kushona na utengenezaji wa
          viatu. Shule mbalimbali zilianzishwa na kugawanywa katika makundi mawili: shule
          za Wamisionari na shule za serikali. Hata hivyo, mtaala wa shule za serikali ulipingwa
          na Wamisionari ambao walitaka utumike mtaala wa shule zao. Elimu ilitolewa kwa
          lugha ya Kiswahili, huku shule za serikali zikihudumia zaidi wavulana na wasichana
          wakibaguliwa. Mfumo huu wa elimu ya kikoloni ulikuwa na idadi ndogo ya wanafunzi
          wa Kiafrika.



                                                  12




                                                                                        03/10/2024   18:15:08
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   12
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   12                                         03/10/2024   18:15:08
   15   16   17   18   19   20   21   22   23   24   25