Page 17 - Historia_Maadili
P. 17

Mfanyabiashara maarufu wa Kiarabu katika njia hii ya kati alikuwa Hemed bin
          Muhammad bin Juma bin Rajab el Murjebi, maarufu kama “Tippu Tip”. Njia kuu ya
          tatu ilikuwa ya Kusini. Njia hii ilianzia Kilwa  Kivinje kuelekea Ziwa Nyasa, kaskazini
          mwa Msumbiji, Malawi na mashariki mwa Zambia. Njia hii ilitawaliwa na Wayao.
          Njia hizi zilitumika kupitisha bidhaa mbalimbali pamoja na misafara ya watumwa.

        FOR ONLINE READING ONLY
          Ukuaji wa kilimo cha mazao ya biashara kama karafuu katika visiwa vya Pemba
          na Unguja na kilimo cha miwa huko Komoro, Ngazija, Mauritius na Reunion,
          ulisababisha ongezeko kubwa la mahitaji ya watumwa kutoka maeneo mbalimbali,
          hasa Tanganyika. Hii ilichangia kukua kwa biashara ya utumwa katika maeneo mengi
          ya eneo hili.

          Kwa ujumla, katika kipindi cha utawala wa Waarabu, uchumi ulikuwa wa kinyonyaji,
          kwani Waarabu walikuwa wanufaika wakuu wa mapato, huku Waafrika wengi
          wakinyonywa kwa kufanya kazi kwa ujira mdogo na wengine wakigeuzwa kuwa
          watumwa. Watumwa hawa waliuzwa na wengine kutumikishwa katika mashamba
          makubwa ya mikarafuu na minazi ya Waarabu huko visiwani Unguja na Pemba.


                              Zoezi la           1.2



           1.  Fafanua  namna  ambavyo  kushamiri  kwa biashara  kulivyoifanya  Zanzibar
               kuwa dola kubwa na kitovu cha biashara katika ukanda wa Afrika Mashariki.
           2.  Eleza mabadiliko ya kiuchumi yaliyoletwa na Waarabu katika jamii za pwani
               ya Tanganyika na Zanzibar.

           3.  Linganisha thamani ya bidhaa zilizobadilishwa kati ya wafanyabiashara wa
               Kiarabu na jamii za pwani ya Tanganyika na Zanzibar.



          Mabadiliko ya kijamii wakati wa utawala wa Waarabu
          Kabla ya kuwasili kwa Waarabu, jamii za pwani ya Tanganyika na Zanzibar zilijengwa
          juu ya maadili yaliyotokana na dini zao za jadi, ambapo baadhi yao waliabudu Mungu
          kupitia miti mikubwa, majabali na mapango makubwa, mito, maziwa na bahari na
          walitoa kafara kwa malengo mbalimbali kulingana na imani zao. Aidha, jamii hizi
          zilijikita katika kutoa  elimu ya jadi ambayo ililenga kumpatia kijana maarifa na
          ujuzi wa kukabiliana na mazingira yake. Hii ilimwezesha kuishi vyema kwa kufuata
          maadili na mila za jamii yake. Kuja kwa Waarabu kulileta mabadiliko makubwa
          katika masuala ya elimu, maadili na utamaduni katika jamii hizi.
          Jamii za pwani ya Tanganyika na Zanzibar zilijifunza lugha ya Kiarabu ili kuimudu dini
          ya Kiislamu na kuendana na matakwa na tamaduni za Waarabu. Hali hii ilisababisha
          watu wengi kujiunga na madrasa kwa ajili ya kujifunza dini ya Kiislamu na lugha


                                                  9




                                                                                        03/10/2024   18:15:07
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   9
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   9                                          03/10/2024   18:15:07
   12   13   14   15   16   17   18   19   20   21   22