Page 12 - Historia_Maadili
P. 12

Waingereza walitawala Tanganyika kuanzia mwaka 1919 hadi 1961. Baada ya Vita
          Kuu ya Kwanza ya Dunia, Tanganyika iliwekwa chini ya udhamini wa Jumuiya ya
          Mataifa (League of Nations) na baada ya Vita Kuu ya
          Pili ya Dunia, chini ya Umoja wa Mataifa (United
          Nations Organisation). Hata hivyo, taasisi hizo ziliipa
          Uingereza mamlaka ya kuitawala  Tanganyika na
        FOR ONLINE READING ONLY
          kuiandaa kujitawala yenyewe. Hivyo, kuanzia mwaka
          1919,  Tanganyika  ilikuwa  chini ya  utawala wa
          Waingereza, ambapo Sir Horace Byatt alikuwa Gavana
          wa kwanza. Kielelezo 1.1 kinaonesha picha ya Gavana
          Sir Horace Byatt.                                      Kielelezo 1.1: Gavana Sir
                                                                       Horace Byatt


          Kuanzia mwaka 1919 hadi 1925, Waingereza waliendeleza muundo wa utawala
          waliourithi kutoka kwa Wajerumani. Hata hivyo, kuanzia mwaka 1926, chini ya
          uongozi wa Gavana Sir Donald Cameron, Waingereza walibadilisha mfumo huo
          na kuanzisha utawala wa kiuwakala. Katika mfumo huu mpya, walitumia mamlaka
          za jadi kutekeleza sera za kikoloni. Tofauti na utawala wa Wajerumani, mfumo
          huu haukuwa na ukatili mkubwa. Mifumo na utawala wa Waarabu, Wajerumani na
          Waingereza imefafanuliwa kwa kina katika sehemu zinazofuata.



                              Zoezi la           1.1

            1.  Kwa nini Waingereza walibadilisha mfumo wa utawala kutoka utawala wa
                moja kwa moja hadi mfumo wa uwakala?

            2.  Eleza jinsi mifumo ya utawala wa Waarabu, Wajerumani na Waingereza
                ilivyoyaathiri maendeleo ya jamii za Kitanzania.

            3.  Tofautisha  mifumo  ya utawala  wa Waarabu, Wajerumani  na Waingereza
                katika Tanzania.


          Utawala wa Waarabu

          Waarabu kutoka Oman walifika Zanzibar na Tanganyika mwishoni mwa karne ya
          18. Kwa madhumuni ya kutawala, walijenga makazi yao katika maeneo ya Unguja,
          Pemba na pwani ya Tanganyika, hususani katika miji ya Kilwa, Tanga na Bagamoyo,
          kama inavyoonyeshwa kwenye Kielelezo 1.2.







                                                  4




                                                                                        03/10/2024   18:15:06
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   4                                          03/10/2024   18:15:06
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   4
   7   8   9   10   11   12   13   14   15   16   17