Page 11 - Historia_Maadili
P. 11

ili kuzipiga jamii zenye nguvu na hivyo kujipenyeza na hatimaye kuimarisha tawala
          zao.

          Mkutano wa Berlin wa mwaka 1884 – 1885, pamoja na mambo mengine, ulilenga
          kuligawanya bara la Afrika miongoni mwa mataifa ya Ulaya bila kujali mipaka
          ya asili ya Waafrika na hivyo kuharakisha ukuaji wa tawala za kikoloni. Hii ilileta
        FOR ONLINE READING ONLY
          madhara makubwa kwa jamii za Kiafrika zilizokuwa zimejengwa katika misingi ya
          utu, umoja, uzalendo na amani. Kukua na kuenea kwa ukoloni kulianza kusababisha
          kuporomoka kwa maadili ya jamii nyingi za Kitanzania. Tamaduni nyingi za asili
          zilianza kufifia kutokana na athari za ukoloni. Kwa mfano, lugha, mila na desturi za
          asili zilianza kupotea au kubadilika kutokana na kuingiliwa, kudumazwa na kubezwa
          na tamaduni za kikoloni.



           Kazi ya kufanya 1.1


           Umeteuliwa kuwa miongoni mwa wanafunzi watakaoshiriki mdahalo wenye mada
           isemayo “Ukoloni ulikuwa na manufaa katika maadili ya jamii za Kitanzania.”
           Soma vitabu na matini mbalimbali kisha andaa dondoo utakazozitumia wakati
           wa mdahalo huo.




          Mifumo ya kikoloni ya mataifa yaliyozitawala jamii za Kitanzania

          Mifumo ya utawala ya Waarabu, Wajerumani na Waingereza katika jamii za Kitanzania
          ilitofautiana kwa kiasi kikubwa, ingawa lengo kuu la mifumo hiyo lilikuwa kunyonya
          na kupora rasilimali watu na rasilimali asilia za jamii za Kitanzania. Waarabu wa
          mwanzo waliofika pwani ya Afrika Mashariki kabla ya karne ya 18, hawakuja kama
          wakoloni bali kama wafanyabiashara. Hata hivyo, Waarabu kupitia utawala wa Sultani
          wa Zanzibar kuanzia karne ya 18, walijikita zaidi katika biashara, hususani biashara
          ya pembe za ndovu, watumwa, karafuu na nazi. Mfumo huu wa utawala ulitengeneza
          tabaka la juu katika jamii, yaani tabaka la Waarabu na Wahindi waliojihusisha na
          kilimo  cha mashamba makubwa na biashara, huku Waafrika wengi wakibaki katika
          hali duni ya kiuchumi, kisiasa na kijamii.

          Wajerumani walitawala jamii za Kitanzania kuanzia mwaka 1885 hadi 1919 baada ya
          Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia. Katika utawala wao, Wajerumani walitumia mfumo
          wa utawala wa moja kwa moja, uliokuwa na matumizi ya nguvu za kijeshi na sheria
          kali dhidi ya watawaliwa. Jamii nyingi za Kitanzania ziliporwa ardhi na kulazimishwa
          kufanya kazi katika mashamba na miradi ya kikoloni kama vile ujenzi wa reli na
          miundombinu mingine kwa ujira mdogo. Wajerumani walitawala nyanja zote za
          maisha ya Waafrika huku wakiendeleza miundombinu kwa ajili ya masilahi yao.




                                                  3




                                                                                        03/10/2024   18:15:06
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   3
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   3                                          03/10/2024   18:15:06
   6   7   8   9   10   11   12   13   14   15   16