Page 8 - Historia_Maadili
P. 8

Dibaji







          Kitabu hiki cha Historia ya Tanzania na Maadili, Shule za Sekondari kimeandikwa
        FOR ONLINE READING ONLY
          mahususi kwa ajili ya mwanafunzi wa Kidato cha Pili katika Jamhuri ya Muungano
          wa Tanzania. Kitabu hiki kimeandaliwa kulingana na Muhtasari wa Somo la Historia
          ya Tanzania na Maadili uliotolewa na Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia wa
          mwaka 2023.

          Kitabu hiki kina sura sita: Ukoloni katika jamii za Kitanzania, Athari za ukoloni
          katika maadili ya Kitanzania, Mapambano ya awali dhidi ya uvamizi wa kikoloni,
          Harakati za kudai uhuru wa Tanganyika na Zanzibar, Ujenzi wa Taifa baada ya ukoloni
          na Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar. Maudhui ya kitabu hiki yamewasilishwa kwa
          njia ya matini, kazi za kufanya, vielelezo, pamoja na picha zinazochochea ujenzi wa
          umahiri unaokusudiwa kwa kila sura. Vilevile, katika kila sura kuna mazoezi yenye
          lengo la kupima na kujenga uelewa pamoja na ujuzi katika somo hili. Hivyo, unapaswa
          kufanya mazoezi na kazi zote zilizopo kwenye kitabu hiki, pamoja na kazi nyingine
          utakazopewa na mwalimu.

          Jifunze zaidi kupitia maktaba mtandao https://ol.tie.go.tz au ol.tie.go.tz














                                                          Taasisi ya Elimu Tanzania
























                                                 viii




                                                                                        03/10/2024   18:15:05
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   8
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   8                                          03/10/2024   18:15:05
   3   4   5   6   7   8   9   10   11   12   13