Page 9 - Historia_Maadili
P. 9

Sura ya Kwanza                         Ukoloni katika jamii
                                                       za Kitanzania



        FOR ONLINE READING ONLY

                   Utangulizi


            Kipindi ukoloni unaingia, jamii nyingi za Kitanzania zilikuwa zimepiga hatua
            katika maendeleo ya kisiasa, kiuchumi na kijamii. Katika sura hii, utajifunza
            kuhusu chimbuko, ukuaji, mifumo na mchango wa ukoloni katika uhusiano
            wa Tanzania na mataifa yaliyoitawala. Umahiri utakaoujenga utakuwezesha
            kuthamini maendeleo ya jamii za Kitanzania katika kipindi cha ukoloni. Pia,
            utaweza kushiriki vyema katika juhudi za kuleta maendeleo ya Tanzania.




                   Fikiri



             Hali ya jamii za Kitanzania wakati ukoloni unaingia.



          Chimbuko na ukuaji wa ukoloni
          Ukoloni ni hali ya nchi moja huitawala nchi nyingine katika nyanja zote za kiuchumi,
          kisiasa na kiutamaduni. Katika muktadha huu, uchumi, siasa na utamaduni wa nchi
          zinazotawaliwa hutumiwa kwa malengo ya wakoloni. Ukoloni ulitokana na kustawi
          kwa mfumo wa ubepari, ambao ulifikia hatua ya ubeberu huko Ulaya  Magharibi.
          Ubeberu huu uliwalazimu wakoloni kuvuka mipaka ya nchi zao ili kutafuta rasilimali
          na masoko mapya ya bidhaa zao na sehemu za kuwekeza mitaji.

          Ukuaji wa ubepari katika robo ya mwisho ya karne ya 19 uliambatana na mapinduzi na
          maendeleo ya viwanda katika nchi za Ulaya Magharibi. Maendeleo hayo ya viwanda
          yalisababisha ongezeko kubwa la mahitaji ya malighafi hasa za kilimo na madini
          kwa ajili ya uzalishaji viwandani. Katika kipindi hicho, malighafi kutoka makoloni
          mengine kama vile Australia, Kanada na Bara la Asia hasa India ya Uingereza (British
          India) hazikutosheleza mahitaji ya viwanda. Baada ya nchi za Ulaya Magharibi
          kutuma wapelelezi miaka ya 1850 hadi 1870 waligundua kuwa Bara la Afrika lina
          uwezo wa kuzalisha malighafi za kutosha kwa ajili ya viwanda vya Ulaya Magharibi.
          Mataifa kama Uingereza, Ufaransa, Ujerumani, Ubelgiji na Ureno yalivutiwa na
          rasilimali hasa ardhi yenye rutuba, misitu, mito, wanyama pori na madini barani
          Afrika.
                                                  1




                                                                                        03/10/2024   18:15:05
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   1                                          03/10/2024   18:15:05
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   1
   4   5   6   7   8   9   10   11   12   13   14