Page 13 - Historia_Maadili
P. 13

FOR ONLINE READING ONLY

































                    Kielelezo 1.2: Maeneo ambayo Waarabu waliweka ngome za utawala wao
          Watawala wa Kiarabu waliotawala pwani ya Afrika Mashariki walifika nchini katika
          vipindi mbalimbali. Wengi wao walivutiwa na utajiri wa rasilimali uliokuwapo katika
          eneo hili. Utajiri huo ulijulikana kutokana na uhusiano wa kibiashara wa muda mrefu
          kati ya pwani ya Afrika Mashariki na nchi za bara la Asia kama vile Omani, Uhindi,
          Uchina na Uajemi.

          Mtawala wa kwanza wa Kiarabu katika eneo hili alijulikana kama Sultani Seyyid Said
          bin Sultan. Sultani huyu alikuwa Mwarabu wa kwanza kutawala kwa pamoja dola za
          Omani na Zanzibar, kuanzia mwanzoni mwa miaka ya 1800 hadi alipofariki dunia
          mwaka 1856. Sultani alivutiwa sana na hali ya hewa ya Zanzibar, pamoja na kustawi
          kwa biashara katika ukanda huo, kina kirefu cha bandari ya Zanzibar na udongo
          wenye rutuba uliostawisha mazao mbalimbali, kama vile mikarafuu na minazi. Hivyo,
          kiongozi huyu aliwahimiza matajiri wa Kiarabu kutoka Omani kuhamia Zanzibar na
          kuanzisha mashamba makubwa ya mikarafuu. Mnamo mwaka 1840, Sultani Seyyid
          Said alihamisha rasmi makao yake kutoka Muscat, Omani hadi Zanzibar na kuifanya



                                                  5




                                                                                        03/10/2024   18:15:06
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   5
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   5                                          03/10/2024   18:15:06
   8   9   10   11   12   13   14   15   16   17   18