Page 25 - Historia_Maadili
P. 25

Kazi ya kufanya 1.5

            Shule yako imealikwa kushiriki mdahalo katika shule ya jirani; andaa hoja
            utakazotumia katika mdahalo huo kuhusu mada inayosomeka, “Utawala
        FOR ONLINE READING ONLY
            wa Waingereza ulikuwa na manufaa makubwa ya kiuchumi katika jamii za
            Tanganyika na Zanzibar.”



          Mabadiliko ya kisiasa wakati wa utawala wa Waingereza
          Baada ya Waingereza kukabidhiwa rasmi madaraka, serikali iliimarisha misingi
          ya utawala kwa kuweka taratibu na sheria ili kurejesha hali ya utulivu iliyotoweka
          wakati wa vita. Awali, Waingereza waliendelea kutumia mtindo wa utawala uliokuwa
          ukitumiwa na Wajerumani. Hata hivyo, baadaye walibadilisha mfumo wa utawala
          kwa kuanza kuwatumia viongozi wa jadi katika shughuli za utawala. Viongozi
          hawa walikuwa na majukumu ya kusimamia maagizo ya serikali, kukusanya kodi,
          kufanya sensa ya watu na mifugo, kuwa na daftari la walipa kodi na kuamua kesi
          zilizofikishwa  katika  mahakama  zao.  Majukumu  haya  yalitekelezwa  chini  ya
          usimamizi wa mabwana shauri wa Kiingereza waliokuwa na jukumu la kufafanua
          sheria za kikoloni kwa wananchi.

          Mtindo wa kisiasa wa kuwatumia machifu ulikuwa ni chombo cha kuendeleza
          mipango ya ukoloni ya kuwakandamiza na kuwanyonya wananchi. Waingereza
          walisisitiza sana ukabila katika mipango yao ili kuwagawa na kuwadhibiti wananchi.
          Kwa mfano, kwenye mashamba na migodi, vibarua walipangiwa mabweni ya kulala
          kwa misingi ya kikabila. Aidha, ubaguzi ulionekana katika shule na hata kwenye
          mashindano ya ngoma na michezo ya jadi.
          Ili kuimarisha utawala wa Waingereza, sheria na kanuni mbalimbali zilitungwa kwa
          lengo la kuwakandamiza wananchi. Sheria zote hizi zililenga kuwanufaisha Wazungu
          na Waasia. Wakoloni walitumia mbinu za kuwalaghai machifu kwa kuunda shirikisho
          la machifu kwa kila kabila na kumteua chifu mmoja kuwa kiongozi mwandamizi wa
          wengine. Kwa mfano, Marealle aliteuliwa kuongoza machifu wa Kichaga, Fundikira
          aliteuliwa kuongoza machifu wa Kinyamwezi,  Makwaia aliteuliwa kuongoza machifu
          wa Kisukuma na Chifu Luther Kingu alichaguliwa kuongoza machifu wa Iramba.

          Waingereza walitumia mtindo wa utawala uliokuwa ukijulikana kama utawala wa
          kiuwakala ulioanzishwa na Gavana Sir Donald Cameron mwaka 1926. Mtindo
          huu uliendeshwa kwa kutumia makamishna wa majimbo na wilaya. Makamishna
          wa wilaya ndio waliokuwa kiungo kati ya serikali ya kikoloni na serikali za mitaa
          zilizoongozwa na machifu wakisaidiwa na majumbe.




                                                  17




                                                                                        03/10/2024   18:15:08
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   17
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   17                                         03/10/2024   18:15:08
   20   21   22   23   24   25   26   27   28   29   30