Page 30 - Historia_Maadili
P. 30

mbinu za kijeshi na kisiasa kutawala jamii za Kitanzania. Hali hii ilileta migongano
          ya mara kwa mara. Wazawa walilazimika kupigania na kulinda ardhi zao, utu na
          uhuru wao dhidi ya utawala wa kigeni. Hali hii lilisababisha uadui kati ya wakoloni
          na jamii mbalimbali za Kitanzania.

          Ukoloni uliathiri kwa kiasi kikubwa uhusiano wa kijamii na kiuchumi wa jamii za
          Kitanzania. Uhusiano wa kibiashara uliokuwa na mafanikio zamani sasa ulibadilika
        FOR ONLINE READING ONLY
          na kuwa wa kiunyonyaji. Wakoloni walipora rasilimali kama vile ardhi na madini
          na kuwanyonya wafanyakazi wa Kitanzania katika mashamba na migodi yao.
          Hii ilisababisha kuongezeka kwa umasikini na ukosefu wa haki miongoni mwa
          Watanzania.
          Mbali na uhasama, ukoloni pia ulileta athari kubwa kwenye utamaduni na mifumo
          ya kijamii. Utamaduni wa kigeni ulienea katika jamii za Kitanzania na kudhoofisha
          utamaduni na maadili ya asili. Hali hii ilichangia kuvunjika kwa mshikamano wa
          kijamii na kuendeleza uhusiano hasi kati ya jamii za Kitanzania na wakoloni.
          Ingawa ukoloni ulisababisha uhusiano mbaya baina yake na jamii za Kitanzania,
          pia ulisababisha mwamko mpya wa utaifa wa kudai uhuru. Harakati za kudai uhuru
          na kujikomboa zilichochea umoja miongoni mwa jamii za Kitanzania. Baada ya
          Tanganyika kupata uhuru mwaka 1961, uhusiano mpya ulijengwa kati ya Tanganyika
          huru na mataifa ya kigeni, yakiwemo mataifa yaliyokuwa yakiitawala. Uhusiano
          huu ulijengwa katika misingi ya kimaadili iliyolenga kuimarisha umoja wa kitaifa,
          kulinda uhuru, kujitegemea na kuheshimu haki za binadamu. Katika kipindi hicho
          cha uhuru wa Tanganyika na mara baada ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar,
          Tanzania ilijipambanua kama taifa lenye msimamo huru katika uhusiano wake na
          mataifa mengine.

                                   Zoezi la marudio


            1.  Eleza sababu za wakoloni kutoanzisha viwanda vya kuzalisha bidhaa katika
                maeneo ya Tanzania wakati wa ukoloni.
            2.  Linganisha  hali  ya  utoaji  wa huduma  za  jamii  wakati  wa  utawala  wa
                Wajerumani na Waingereza katika jamii za Kitanzania.

            3.  Fafanua namna ambavyo sera za utawala wa Wajerumani na Waingereza
                zilivyokinzana na maadili ya jamii za Kitanzania.
            4.  Jamii za sasa za Tanzania zinaweza kujifunza nini kuhusu usimamizi wa
                rasilimali na utawala kutoka kwa Wajerumani na Waingereza?
            5.  Kwa kurejelea utoaji wa huduma za kijamii wakati wa ukoloni, pendekeza
                namna bora ya kuboresha utoaji wa huduma za kijamii katika Tanzania ya
                sasa.
            6.  Tofautisha utoaji wa huduma za jamii wakati wa sasa na ule wa utawala wa
                Wajerumani na Waingereza.


                                                  22




                                                                                        03/10/2024   18:15:09
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   22                                         03/10/2024   18:15:09
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   22
   25   26   27   28   29   30   31   32   33   34   35