Page 26 - Historia_Maadili
P. 26

Baada ya Vita Kuu ya Pili ya Dunia, Waingereza walipanua Baraza la Kutunga
          Sheria. Baraza hili lilikuwa na kazi ya kumshauri Gavana kuhusu masuala mbalimbali
          yanayohusu utawala. Jukumu jingine la baraza lilikuwa ni kutunga sheria ambazo
          zilihitaji idhini kutoka serikali ya Uingereza kabla ya kutumika. Wajumbe wa Baraza
          la Kutunga Sheria waliingia kwa kuteuliwa na Gavana mwenyewe, huku wengine
          wakiteuliwa kutokana na nyadhifa zao serikalini. Baraza hili kwa mara ya kwanza
        FOR ONLINE READING ONLY
          lilijumuisha machifu wa Kitanganyika, wakiwemo Chifu Abdieli Shangali na Chifu
          Kidaha Makwaia.

          Zanzibar ilikuwa na uhusiano maalumu na Waingereza, lakini kwa hali halisi, siasa
          ya Waingereza iliifanya Zanzibar kuwa koloni. Ingawa Waingereza waliutumia
          utawala wa Sultani katika kuitawala Zanzibar, utawala wa Kisultani haukujitegemea
          hata mara moja. Mwanzoni mwa mwaka 1914, Baraza la Ushauri lilianzishwa kwa
          lengo la kumshauri Sultani na serikali yake kuhusu masuala ya serikali. Unguja na
          Pemba ziligawanywa katika wilaya, mudiria na shehia. Kila wilaya ilikuwa chini
          ya afisa wa serikali ambaye alikuwa Mwingereza, huku Mudir na Sheha wa Kiarabu
          wakisimamia mudiria na shehia. Hata hivyo, kulikuwa na Waafrika wachache
          waliokuwa wakisimamia shehia, lakini walipewa jukumu la kuwahimiza wenzao
          kuwatumikia Wazungu, Waarabu na Wahindi.

                              Zoezi la          1.5


           1.  Tofautisha mfumo wa utawala wa Waingereza na ule wa Wajerumani katika
                kuzitawala jamii za Kitanzania.
           2.  Eleza kwa kifupi majukumu ya viongozi wa jadi katika serikali ya Kiingereza.

           3.  Linganisha majukumu ya viongozi wa sasa wa serikali za mitaa na yale ya
                viongozi wa jadi wakati wa utawala wa Waingereza Tanganyika.
           4.  Tofautisha utawala wa Waingereza Tanganyika na Zanzibar.



          Mabadiliko ya kijamii wakati wa utawala wa Waingereza

          Mabadiliko ya kijamii wakati wa utawala wa Waingereza yalijikita zaidi katika utoaji
          wa huduma za msingi kama elimu, afya, maji, umeme na miundombinu. Huduma
          hizi zilitolewa kwa madhumuni ya kuiwezesha serikali ya Waingereza kurahisisha
          utekelezaji wa malengo ya kikoloni, ikiwemo kupata nguvukazi ya kutosha miongoni
          mwa wananchi ili kuwezesha uzalishaji wa malighafi muhimu kwa viwanda vyao huko
          Ulaya. Kwa kiasi kikubwa, huduma za jamii zilizoanzishwa na serikali ya kikoloni
          hazikulenga kuwahudumia wananchi bali kutimiza masilahi ya wakoloni.

          Elimu: Shughuli za utoaji wa elimu ziliathirika sana wakati wa Vita Kuu ya Kwanza
          ya Dunia. Serikali ya Uingereza, kwa kushirikiana na mashirika ya dini, ilianza
          kutoa elimu kwa wananchi kwa kufuata mipango na mahitaji ya wakoloni. Sehemu
                                                  18




                                                                                        03/10/2024   18:15:08
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   18                                         03/10/2024   18:15:08
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   18
   21   22   23   24   25   26   27   28   29   30   31