Page 27 - Historia_Maadili
P. 27

zilizopewa kipaumbele ni zile zilizozalisha mazao ya biashara, hususani kahawa na
          pamba, pamoja na vituo vya wamisionari. Kwa mfano, shule nyingi katika Tanganyika
          zilijengwa katika maeneo ya  Kilimanjaro na Bukoba.


          Malengo ya elimu iliyotolewa na Waingereza yalikuwa kuwapatia wananchi maarifa
          yatakayowasaidia kuendeleza mipango na mikakati ya kikoloni. Hii ilifanywa kwa
        FOR ONLINE READING ONLY
          kuwapa wananchi elimu ya mbinu bora za kilimo na ufugaji na elimu ya afya. Pia,
          iliwaandaa mabwanyenye uchwara ambao walisaidia kuongoza na kufundisha utii
          na unyenyekevu ili kutekeleza maagizo na maelekezo ya serikali ya kikoloni. Elimu
          ilitolewa katika ngazi zifuatazo: elimu ya msingi (darasa la 1- 4), elimu ya kati
          (darasa la 5-8) na elimu ya sekondari (darasa la 9-12). Mtaala wa elimu ulijikita
          zaidi katika kufundisha mambo ya kigeni, hivyo maudhui yaliyofundishwa shuleni
          hayakuwasaidia wananchi kutatua matatizo yao ya kila siku. Kwa mfano, wanafunzi
          walifundishwa kuhusu mila, tamaduni na desturi za Kiingereza badala ya mila zao
          za asili.

          Kwa upande wa Zanzibar, Waingereza walitoa elimu iliyoendeleza matabaka ya
          kijamii. Wazanzibari walifundishwa jinsi ya kuwa watiifu na waaminifu kwa Sultani
          na viongozi wao, ambao wengi walikuwa Waarabu. Waarabu walipewa elimu maalumu
          iliyowawezesha kuendelea kujiona kuwa bora kuliko Waafrika. Ubaguzi huu katika
          utoaji wa elimu ulikuwa kikwazo kikubwa kwa Watanganyika na Wazanzibari.

          Aidha, ubaguzi wa kikanda na kimaeneo ulikuwa dhahiri katika mfumo wa elimu,
          ambapo shule nyingi zilijengwa katika maeneo ya uzalishaji mali kama Moshi,
          Bukoba, Mbeya na Mwanza. Maeneo ya Rukwa na Kigoma yalikuwa na shule chache
          kwa kuwa hayakuwa maeneo ya uzalishaji mali. Hivyo, wananchi wa maeneo haya
          walinyimwa fursa za elimu. Wananchi hawa waliendelea kwenda kufanya kazi
          za manamba katika mashamba na migodi ya kikoloni. Hivyo, elimu iliyotolewa
          iliwafaidisha wachache pekee kwani hata shule zilikuwa chache na zilitoa elimu
          kwa watoto wa machifu. Kwa mfano, Shule ya Wavulana Tabora ilikuwa maalumu
          kwa watoto wa machifu.

          Afya: Huduma za afya wakati wa utawala wa Waingereza zilitolewa kwa lengo la
          kuziendeleza na kuzilinda afya za wananchi ili wawe na nguvu za kushiriki kikamilifu
          katika shughuli za kuendeleza uchumi wa kikoloni. Pamoja na kwamba Waingereza
          walihitaji nguvukazi yenye afya, bado huduma za afya zilikuwa chache na duni.
          Sehemu zilizopata huduma za afya ni zile zilizo kwenye maeneo ya uzalishaji mali,
          makazi ya walowezi na vituo vya wamisionari.

          Kama ilivyokuwa katika elimu, huduma za afya pia zilitolewa kwa misingi ya ubaguzi
          wa rangi. Huduma bora zaidi zilitolewa kwa Wazungu, wakifuatiwa na Waasia, huku
          Waafrika wakipewa huduma za kiwango cha chini. Waingereza hawakuwaandaa
          Waafrika kuwa matabibu wa ngazi za juu, bali walifundishwa kuwa matabibu wa
          ngazi za chini. Vilevile, hospitali na vituo vya afya vilifuata misingi hiyo ya ubaguzi,

                                                  19




                                                                                        03/10/2024   18:15:08
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   19                                         03/10/2024   18:15:08
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   19
   22   23   24   25   26   27   28   29   30   31   32