Page 37 - Historia_Maadili
P. 37

Halikadhalika, miongoni mwa jamii ya  Wasukuma, mavazi ya kitamaduni
          yalitengenezwa kwa ngozi ya wanyama na nyuzi za mimea kabla ya kuanzishwa
          kwa nguo za kufuma. Wanawake pia walivaa sketi za nyasi zilizotengenezwa kwa
          nyuzi za mimea. Mavazi haya yalikuwa rahisi lakini yalilingana na mazingira na hali
          ya hewa ya Usukumani. Aidha, nguo hizo ziliakisi shughuli za kilimo na ufugaji ya
          jamii ya Wasukuma. Mavazi pia yaliendana na mitindo ya urembo mathalani mitindo
        FOR ONLINE READING ONLY
          ya kusuka nywele kwa wanawake na kunyoa nywele kwa wanaume kwa mfano kwa
          jamii ya Wanyamwezi kama inavyoonekana katika Kielelezo 2.2. Kwa ushawishi
          wa kikoloni, nguo za pamba zikawa za kawaida zaidi na mavazi ya jadi kama vile
          kaniki yalianza kuhifadhiwa kwa matukio maalumu. Kielelezo 2.1 kinaonesha vazi
          la asili la kaniki la jamii ya Wasukuma.




















              Kielelezo 2.1: Vazi la asili        Kielelezo 2.2: Mitindo ya nywele katika
               katika jamii ya Wasukuma                  jamii ya Wanyamwezi

          Jamii za Wanyamwezi, Wasukuma, Wahehe, Wachaga, Wahaya na Wasambaa zilikuwa
          na utofauti wa mavazi kati ya wananchi na watawala wao. Kulikuwa na nguo maalumu
          zilizovaliwa na watawala ili kuonesha mamlaka yao. Mavazi hayo ni pamoja na nguo
          za ngozi za wanyama hasa simba na chui, kofia, regalia, taji, mapambo na mkoba.
          Mavazi haya yaliandamana na vifaa kama usinga, ngao na mkuki kama alama za
          nguvu, mamlaka na utawala wa eneo la kiongozi. Pia, kulikuwa na nguo maalumu
          zilizovaliwa na wazee walioongoza kufanya matambiko ya kijamii. Nguo hizi zilikuwa
          na rangi maalumu. Nguo nyeupe na nyeusi ndio ziliruhusiwa kwa ajili ya matambiko.
          Nguo nyekundu hazikuruhusiwa kutumika katika matambiko.

          Mavazi na mitindo ya kikoloni iliingia na kuenea katika jamii za Kitanzania.
          Wamisionari, maofisa wa kikoloni na wafanyabiashara walileta aina mpya za nguo
          kama vile suruali, mashati, gauni na suti. Vilevile, katika maeneo ya pwani na vituo
          vya kibiashara kama Ujiji na Tabora, ambako biashara zilifanyika kati ya jamii za
          Kitanzania na Waarabu, mavazi kama kanzu, baibui, makubadhi na vikoi yalikuwa



                                                  29




                                                                                        03/10/2024   18:15:10
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   29                                         03/10/2024   18:15:10
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   29
   32   33   34   35   36   37   38   39   40   41   42