Page 41 - Historia_Maadili
P. 41

mkubwa ikienea maeneo mengi nchini na idadi ya waumini ikaongezeka. Waumini
          wapya walionekana kujitolea kwa imani yao, wakichukua nafasi za uongozi katika
          jamii na kusaidia kuendeleza mafundisho mapya.

          Mbali na Watanzania wengi kuingia kwenye dini ya Kikristo, mabadiliko ya dini
          yalisababisha pia mabadiliko katika maadili na taratibu za Kitanzania, kama vile
        FOR ONLINE READING ONLY
          masuala ya ndoa, tohara, mavazi, vyakula na muziki. Desturi na mila za Kitanzania

          zilipuuzwa na badala yake, desturi na mila za kigeni zikapewa umuhimu mkubwa.
          Hii ilisababisha mkanganyiko katika kulea watoto kati ya utamaduni wa Kitanzania
          na mafundisho ya Kikristo.

          Muingiliano na uhusiano wa dini na ukoloni pia ulisababisha mgawanyiko katika
          jamii ya Kitanzania. Baadhi ya watu waliokubaliana na utamaduni wa kikoloni
          walionekana kama wasaliti wa imani na maadili ya Kitanzania. Vilevile, kulikuwa na
          wale waliopinga mabadiliko haya ya kikoloni, wakidai kwamba utamaduni na hasa
          imani za asili, zinahitaji kulindwa na kuheshimiwa. Hivyo, kukandamizwa kwa dini

          za jadi kulichangia kuzizorotesha, kwani vizazi vipya vilihimizwa kufuata Ukristo
          au Uislamu. Hii ilisababisha upotevu wa maarifa na desturi za kiutamaduni ambazo
          kwa muda mrefu zilikuwa muhimu kwa mfumo wa kijamii wa jamii za Kitanzania.

                              Zoezi la          2.3



            1.  Bainisha athari zingine zilizoletwa na Ukristo nchini Tanzania.
            2.  Linganisha mfumo wa elimu ya jadi na mfumo wa elimu ya sasa.
            3.  Eleza  mchango wa dini za jadi katika  kulinda na kudumisha maadili  ya
               Kitanzania.

            4.  Fafanua umuhimu wa tiba za asili katika mazingira ya sasa ya Kitanzania.


          Lugha: Kabla ya ukoloni, jamii za Kitanzania zilizungumza lugha za kiasili kama
          vile Kimasai, Kisukuma, Kichaga, Kizigua, Kizaramo, Kidigo, Kimwera, Kitumbatu
          na nyinginezo nyingi. Lugha hizi hazikuwa tu njia za mawasiliano, bali pia zilibeba
          utamaduni, utambulisho, mila, desturi, miiko na kumbukumbu katika jamii iliyohusika.
          Hata hivyo, mifumo ya elimu ya kikoloni ilileta mabadiliko makubwa kwenye lugha
          za asili. Lugha kama Kiingereza kilianza kutumika kama lugha ya kufundishia shuleni,
          hali iliyosababisha kupungua kwa matumizi ya lugha za asili. Moja ya athari kubwa
          ilikuwa ni kushinikiza matumizi ya lugha za kikoloni hivyo kusababisha kupungua
          kwa matumizi ya lugha za asili. Jamii zilianza kuwaona wasomi wanaozungumza
          Kiingereza kama kipimo cha usomi na ustaarabu. Watu wasiojua kuandika na
          kuzungumza Kiingereza walionekana kuwa si wasomi na wastaarabu. Usomi na


                                                  33




                                                                                        03/10/2024   18:15:10
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   33                                         03/10/2024   18:15:10
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   33
   36   37   38   39   40   41   42   43   44   45   46