Page 51 - Historia_Maadili
P. 51

Mapambano haya yalilenga kuzuia kuingizwa kwa maadili ya kikoloni katika jamii za
          Kitanzania. Jamii hizi zilikuwa na maadili, mila na desturi zilizowiana na mazingira
          yao, pamoja na lugha, ngoma na imani za kidini (dini za jadi). Kila jamii ilikuwa na
          imani katika Mungu, ambaye alitambulika kwa majina mbalimbali ya kijadi kama vile
          Mlungu, Mnungu (kwa Wazigua), Kyala (kwa Wanyakyusa), Ruwa (kwa Wachaga)
          na Ngai (kwa Wamasai).
        FOR ONLINE READING ONLY
          Hata hivyo, baada ya kuingia kwa wakoloni na kuanzisha utawala wao, utamaduni na
          maadili ya jamii za Kitanzania yalidhoofishwa na kutajwa kuwa ya kishenzi. Wakoloni
          walileta utamaduni kutoka katika mataifa yao uliosisitiza maadili ya kibepari, ikiwa
          ni pamoja na ubaguzi wa rangi, uporaji, ukatili, unyonyaji, unyanyasaji, matabaka na
          ubinafsi. Pia, walileta maadili ya dini za kigeni (Ukristo na Uislamu) ambayo mara
          nyingi yalipingana na maadili ya dini za jadi.



           Kazi ya kufanya 3.1


            Soma matini kutoka vyanzo mbalimbali na ubainishe tofauti ya uvamizi
            uliokuwepo kati ya Afrika Mashariki ya Kijerumani (Tanganyika) na Zanzibar.





           Kazi ya kufanya 3.2


            Kwa kutumia taarifa kutoka vyanzo mbalimbali fanya uchunguzi kuhusu Karl
            Peters alivyoingia mikataba ya kilaghai. Andika insha yenye maneno mia tatu
            (300) ukiwashauri viongozi wa kizazi cha sasa kipi cha kujifunza kutokana na
            mikataba ya Karl Peters.




                              Zoezi la          3.1


            1.  Eleza dhana ya mtawala na mtawaliwa.

            2.  Tofautisha  utawala  wa  Waarabu  Zanzibar  na ule  wa  Wajerumani  katika
               Afrika Mashariki ya Kijerumani.

            3.  Fafanua mbinu zilizotumiwa na wakoloni kuanzisha utawala wa kikoloni
               Tanganyika.
            4.  Eleza namna maadili ya kibepari yanavyoendelea kuathiri maadili ya jamii
               za Kitanzania wakati wa sasa.





                                                  43




                                                                                        03/10/2024   18:15:12
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   43                                         03/10/2024   18:15:12
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   43
   46   47   48   49   50   51   52   53   54   55   56