Page 107 - Historia_Maadili
P. 107
Ujenzi wa maadili
Mapinduzi ya Zanzibar yalileta ukomo wa matabaka yaliyokuwapo kati ya Waarabu,
Wahindi na Waafrika. Kwa kuondoa mfumo wa ubaguzi na ukandamizaji, Mapinduzi
haya yaliweka misingi wa usawa wa kijamii, ambapo watu wote walihesabiwa kuwa
na thamani sawa bila kujali asili yao. Hii ilijenga mazingira ya usawa, upendo, amani,
FOR ONLINE READING ONLY
heshima na mshikamano miongoni mwa watu wote. Serikali mpya ilisisitiza umuhimu
wa demokrasia, haki za binadamu, utu, usawa na ustawi wa watu. Hii ilichangia katika
kuhifadhi maadili ya jamii kama vile ushirikiano, usawa, kuheshimiana na kusaidiana
ambayo ni sehemu muhimu ya utamaduni na utambulisho wa Mzanzibari.
Sambamba na hayo, Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar yalichangia kukuza na
kuendeleza lugha ya Kiswahili. Baada ya Mapinduzi, serikali mpya ilitilia mkazo
umuhimu wa Kiswahili kama nyenzo muhimu ya kujenga umoja na utambulisho wa
kitaifa. Kiswahili kikawa lugha rasmi ya serikali na wananchi wote wa Zanzibar.
Ili kuhakikisha lugha hii inakua na kustawi, vilianzishwa vyombo mbalimbali vya
habari kama vile magazeti ya Kiswahili, redio na baadaye vipindi vya televisheni.
Pia, taasisi na wasomi walihimizwa kusoma na kuandika makala mbalimbali kwa
kutumia lugha hii. Jambo hilo lilisababisha kuandikwa kwa kamusi na vitabu vya
sarufi. Vitabu hivi vilikuwa nyenzo za elimu kwa lengo la kukuza Kiswahili katika
maeneo mengine ya Afrika Mashariki na bara zima la Afrika.
Serikali ilihamasisha matamasha mbalimbali ya kitamaduni ili kuimarisha umoja na
mshikamano wa Wazanzibari. Kwa mfano, kuna matamasha kama Sauti za Busara,
Sherehe za Mwaka Kogwa, Tamasha la Nchi za Jahazi Zanzibar (ZIFF), Tamasha
la Vyakula vya Asili Makunduchi na mashindano ya mpira wa miguu ya Kombe la
Mapinduzi. Haya matamasha yamesaidia na yanaendelea kusaidia, katika kuelimisha
kizazi kipya kuhusu maadili, urithi wa kitamaduni na umuhimu wa kuuhifadhi.
Zoezi la 6.4
1. Bainisha jitihada zingine zilizochukuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya
Zanzibar katika kuujenga umoja, usawa na mshikamano kwa jamii za
Wazanzibari.
2. Eleza ni kwa namna gani lugha ya Kiswahili imefanikiwa kuwaunganisha
Wazanzibari baada ya Mapinduzi.
3. Fafanua namna Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar yanavyoenziwa katika
jamii ya sasa ya Watanzania.
99
03/10/2024 18:15:20
HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd 99
HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd 99 03/10/2024 18:15:20

