Page 87 - Fasihi ya Kiswahili kwa Shule za Sekondari Kiongozi cha Mwalimu Kidato cha Tano
P. 87

Fasihi ya Kiswahili  Shule za Sekondari


           Shughuli ya 6.12
           Hatua za ufundishaji

             (i)   Andaa  mazingira  ya  kufanyika  kwa shindano  la  utunzi  wa
           FOR ONLINE READING ONLY
                  hadithi za watoto.
             (ii)  Waongoze wanafunzi kutunga hadithi za watoto. Kila
                  mwanafunzi achague mada moja kati ya zile zilizobainishwa
                  kwenye Kitabu cha Mwanafunzi. Kuweka vigezo vya ushindani
                  kwa kuzingatia hatua na kanuni za utunzi wa hadithi za watoto.
                  Unaweza kufuata hatua zifuatazo:
                  •    Kutoa muda wa utungaji unaweza kuwa wiki mbili hadi
                       tatu;

                  •    Kukusanya hadithi hizo;
                  •    Kuandaa jopo la majaji watakaotathmini  kazi hizo
                       (wanaweza kuwa walimu, wanafunzi wenzao au wataalamu
                       wengine wa fasihi);

                  •    Kuandaa na kupitia vigezo vya kutathmini hadithi hizo;

                  •    Kuanza mchakato wa kutathmini; na
                  •    Kutangaza washindi.

             (iii)  Waelekeze  wanafunzi kufanya tamrini  iliyomo  kwenye
                  Kitabu cha Mwanafunzi, kisha sahihisha na kuondoa makosa
                  yanayoweza kujitokeza.

           Majibu

           Majibu ya tamrini  yatategemeana  na uelewa  wa mwanafunzi.  Pia,
           unaweza kupima namna mwanafunzi anavyoweza kuhawilisha maarifa
           na kuyaweka katika mazingira na maisha halisi.









                 Kiongozi cha Mwalimu                                    81
                    Kidato cha Tano



                                                                            23/06/2024   17:48
     FASIHI YA KISWAHILI KIONGOZI  CHA MWALIMU KIDATO CHA TANO.indd   81    23/06/2024   17:48
     FASIHI YA KISWAHILI KIONGOZI  CHA MWALIMU KIDATO CHA TANO.indd   81
   82   83   84   85   86   87   88