Page 82 - Fasihi ya Kiswahili kwa Shule za Sekondari Kiongozi cha Mwalimu Kidato cha Tano
P. 82

Fasihi ya Kiswahili  Shule za Sekondari


             (iii)  Rekebisha upungufu unaojitokeza  wakati wa majadiliano na
                  uwasilishaji ili kuondoa dosari zinazojitokeza.

             (iv)  Waelekeze  wanafunzi kufanya zoezi la 6.2 lililomo kwenye
                  Kitabu cha Mwanafunzi, kisha sahihisha na kuondoa makosa
           FOR ONLINE READING ONLY
                  yatakayojitokeza.

           Majibu

           Majibu ya shughuli 6.6 yanaweza kutokana na uelewa wa mwanafunzi.
           Pamoja na yale yaliyopo kwenye Kitabu cha Mwanafunzi. Pia, majibu
           ya zoezi la 6.2 yatatokana na uelewa wa mwanafunzi


             Somo la 5: Kanuni za utunzi na kutunga maigizo


           Shughuli ya 6.7 (a)

           Hatua za ufundishaji

             (i)   Tumia njia ya bungua bongo kuwaongoza wanafunzi kueleza
                  tofauti kati ya hatua na kanuni za utunzi.

             (ii)  Waongoze wanafunzi kufanya shughuli ya 6.7 (a) iliyomo
                  kwenye Kitabu cha Mwanafunzi.

             (iii)  Waelekeze wanafunzi kuunda vikundi vitatu wakiwa darasani.
                  Kikundi cha kwanza kijadili kuhusu maana ya maigizo, kikundi
                  cha pili kijadili kuhusu kanuni za utunzi wa maigizo na kikundi
                  cha tatu kijadili kuhusu umuhimu wa maigizo. Hakikisha kila
                  mwanafunzi anashiriki katika kutoa mawazo yake. Tembelea
                  kila kikundi ili kurekebisha dosari zinazojitokeza katika
                  majadiliano.

             (iv)  Waongoze wanafunzi kufanya uwasilishaji, kila kikundi
                  kichague mwakilishi awasilishe kazi yao na wanafunzi wengine
                  washiriki kuchangia hoja na kuuliza maswali. Rekebisha dosari
                  zinazojitokeza katika uwasilishaji.


             76                                        Kiongozi cha Mwalimu
                                                          Kidato cha Tano



                                                                            23/06/2024   17:48
     FASIHI YA KISWAHILI KIONGOZI  CHA MWALIMU KIDATO CHA TANO.indd   76
     FASIHI YA KISWAHILI KIONGOZI  CHA MWALIMU KIDATO CHA TANO.indd   76    23/06/2024   17:48
   77   78   79   80   81   82   83   84   85   86   87