Page 81 - Fasihi ya Kiswahili kwa Shule za Sekondari Kiongozi cha Mwalimu Kidato cha Tano
P. 81
Fasihi ya Kiswahili Shule za Sekondari
(i) Waelekeze wanafunzi kufanya zoezi la 6.2 lililomo kwenye
Kitabu cha Mwanafunzi, kisha sahihisha na utoe mrejesho.
Somo la 4: Hatua za utunzi wa kazi za kifasihi
FOR ONLINE READING ONLY
Shughuli ya 6.5
Hatua za ufundishaji
(i) Waongoze wanafunzi kufanya shughuli ya 6.5 iliyomo kwenye
Kitabu cha Mwanafunzi.
(ii) Waelekeze wanafunzi kupakua, kusoma na kueleza hatua za
utunzi wa kazi za fasihi. Waulize maswali wanafunzi kupima
uelewa wao kuhusu hatua hizo.
(iii) Waelekeze wanafunzi kukaa katika vikundi na kujadili hatua za
utunzi wa kazi za fasihi, hakikisha kila mwanafunzi anashiriki
katika kutoa mawazo yake. Aidha, kutoka katika kila kikundi,
chagua mwakilishi awasilishe kazi yao na wanafunzi wengine
washiriki kuchangia hoja na kuuliza maswali. Rekebisha dosari
zinazojitokeza katika majadiliano na uwasilishaji.
Majibu
Majibu ya shughuli ya 6.5 yanaweza kuwa yale yaliyopo kwenye Kitabu
cha Mwanafunzi pamoja na yanayotokana na uelewa wa mwanafunzi.
Shughuli ya 6.6
Hatua za ufundishaji
(i) Waongoze wanafunzi kwa njia ya maswali na majibu kuibua
umuhimu wa kuzingatia hatua za utunzi.
(ii) Waongoze wanafunzi kukaa katika vikundi na kujadili
shughuli ya 6.6 iliyomo kwenye Kitabu cha Mwanafunzi, kisha
kuwasilisha kwa ajili ya majadiliano zaidi.
Kiongozi cha Mwalimu 75
Kidato cha Tano
23/06/2024 17:48
FASIHI YA KISWAHILI KIONGOZI CHA MWALIMU KIDATO CHA TANO.indd 75 23/06/2024 17:48
FASIHI YA KISWAHILI KIONGOZI CHA MWALIMU KIDATO CHA TANO.indd 75