Page 77 - Fasihi ya Kiswahili kwa Shule za Sekondari Kiongozi cha Mwalimu Kidato cha Tano
P. 77
Fasihi ya Kiswahili Shule za Sekondari
(f) Kuchambua kanuni za utunzi na kutunga mashairi; na
(g) Kuchambua kanuni za utunzi na kutunga na hadithi za watoto.
Mahitaji
FOR ONLINE READING ONLY
Matini na makala za kifasihi, kamusi, magazeti, hadithi, nyimbo,
mashairi na maigizo yaliyorekodiwa.
Somo la 1: Miktadha inayochagiza utunzi wa kazi za fasihi
Shughuli ya 6.1 (a)
Hatua za ufundishaji
(i) Kwa njia ya maswali na majibu waongoze wanafunzi kuibua
masuala yanayohusiana na utunzi wa kazi za kifasihi.
(ii) Waelekeze wanafunzi kukaa katika vikundi na kujadili shughuli
ya 6.1(a) iliyomo kwenye Kitabu cha Mwanafunzi, kisha
kuwasilisha hoja zao kwa ajili ya majadiliano zaidi.
Majibu
Majibu ya shughuli ya 6.1 (a) yatatokana na uelewa wa mwanafunzi.
Katika shughuli 6.1 (a), mwanafunzi aeleze miktadha inayochangia
utunzi wa kazi za fasihi.
Shughuli ya 6.1 (b)
Hatua za ufundishaji
(i) Waelekeze wanafunzi kukusanya kazi mbalimbali za fasihi.
Kwa njia ya maswali na majibu, waongoze kuchambua kuwapo
tofauti mbalimbali za kuibuliwa kwa kazi hizo.
(ii) Waongoze wanafunzi kukaa katika vikundi na kujadili
shughuli ya 6.1(b) iliyomo kwenye Kitabu cha Mwanafunzi,
kisha kuwasilisha hoja zao kwa ajili ya majadiliano zaidi.
Kiongozi cha Mwalimu 71
Kidato cha Tano
23/06/2024 17:48
FASIHI YA KISWAHILI KIONGOZI CHA MWALIMU KIDATO CHA TANO.indd 71 23/06/2024 17:48
FASIHI YA KISWAHILI KIONGOZI CHA MWALIMU KIDATO CHA TANO.indd 71