Page 78 - Fasihi ya Kiswahili kwa Shule za Sekondari Kiongozi cha Mwalimu Kidato cha Tano
P. 78

Fasihi ya Kiswahili  Shule za Sekondari


                  Katika uwasilishaji waulize wanafunzi maswali kujua kama
                  wameelewa na sahihisha upungufu unaojitokeza.

           Majibu

           FOR ONLINE READING ONLY
           Majibu ya shughuli ya 6.1 (b) yatatokana na uelewa wa mwanafunzi.
           Katika shughuli hii, mwanafunzi achambue miktadha iliyooibua kazi
           alizozikusanya. Pia, unaweza kumrejesha mwanafunzi katika mazingira
           yake ya kawaida kwa kumuuliza kama akitaka kutunga kazi ya fasihi
           nini kitamsukuma na kuchochea uteuzi wa mada.

             (i)   Waelekeze  wanafunzi kufanya zoezi la 6.1 lililomo kwenye
                  Kitabu cha Mwanafunzi, kisha sahihisha na kuondoa makosa
                  yanayojitokeza.


             Somo la 2:  Fursa mbalimbali zinazotokana na kazi za kifasihi
                        za Kiswahili


           Shughuli ya 6.2
           Hatua za ufundishaji


             (i)   Kwa njia  ya  bungua  bongo,  waongoze  wanafunzi  kutambua
                  dhana ya fursa katika muktadha wa kazi za fasihi.

             (ii)  Waongoze  wanafunzi  kukaa  katika  vikundi  kujadili  fursa
                  zinazotokana  na  kazi  ya  fasihi.  Wanafunzi  wabandike  kazi
                  za kila kikundi kwenye ukuta wa darasa, kisha wanafunzi
                  wazitembelee na kuzisoma kwa kupokezana.

             (iii)  Waongoze wanafunzi kuuliza maswali ili kupima uelewa wa
                  wanafunzi na kutoa ufafanuzi kwenye hoja zinazowatatiza, kisha
                  toa ufupisho wa kile walichokuwa wakijadiliana wanafunzi.









             72                                        Kiongozi cha Mwalimu
                                                          Kidato cha Tano



                                                                            23/06/2024   17:48
     FASIHI YA KISWAHILI KIONGOZI  CHA MWALIMU KIDATO CHA TANO.indd   72
     FASIHI YA KISWAHILI KIONGOZI  CHA MWALIMU KIDATO CHA TANO.indd   72    23/06/2024   17:48
   73   74   75   76   77   78   79   80   81   82   83