Page 74 - Fasihi ya Kiswahili kwa Shule za Sekondari Kiongozi cha Mwalimu Kidato cha Tano
P. 74
Fasihi ya Kiswahili Shule za Sekondari
(ii) Waelekeze wanafunzi kukaa katika vikundi vinne, kila kikundi
kichague mada moja kati ya hizo zilizoorodheshwa kwenye
Kitabu cha Mwanafunzi, kisha kutunga malumbano ya hoja
kwa kutumia maarifa ya kifasihi ili kuwasilisha hoja zenye
FOR ONLINE READING ONLY
mantiki na ushawishi. Hakikisha kila mwanafunzi anashiriki
kikamilifu. Rekebisha dosari zinazojitokeza.
(iii) Waongoze wanafunzi kuandaa uwasilishaji. Kila kikundi
kiwasilishe malumbano ya hoja kulingana na mada
waliyopangiwa. Hakikisha kila mwanafunzi anashiriki kwa
kutoa maoni au kuuliza maswali ili kuboresha kazi ya kikundi
husika. Sahihisha upungufu unaojitokeza katika uwasilishaji,
kisha toa mrejesho.
Majibu
Majibu ya shughuli ya 5.13 yatategemea uelewa wa mwanafunzi kwa
kuzingatia mada aliyoichagua. Katika utunzi wa malumbano hayo,
mwanafunzi aoneshe namna anyowasilisha hoja zenye mantiki na
ushawishi.
Shughuli ya 5.14
Hatua za ufundishaji
(i) Waongoze wanafunzi kufanya shughuli ya 5.14 iliyomo kwenye
Kitabu cha Mwanafunzi.
(ii) Waongoze wanafunzi kuchagua mada yoyote anayoipenda,
kisha kutunga malumbano ya hoja kwa kutumia maarifa ya
kifasihi ili kuwasilisha hoja zenye mantiki na ushawishi.
Hakikisha kila mwanafunzi anashiriki kikamilifu. Rekebisha
dosari zinazojitokeza.
(iii) Kusanya na sahihisha kazi za wanafunzi ili kuondoa upungufu
unaojitokeza.
68 Kiongozi cha Mwalimu
Kidato cha Tano
23/06/2024 17:48
FASIHI YA KISWAHILI KIONGOZI CHA MWALIMU KIDATO CHA TANO.indd 68 23/06/2024 17:48
FASIHI YA KISWAHILI KIONGOZI CHA MWALIMU KIDATO CHA TANO.indd 68