Page 71 - Fasihi ya Kiswahili kwa Shule za Sekondari Kiongozi cha Mwalimu Kidato cha Tano
P. 71

Fasihi ya Kiswahili  Shule za Sekondari


             (ii)  Waongoze wanafunzi kuchambua  hoja zenye mantiki na
                  ushawishi kuhusu ujenzi wa wahusika kutoka katika kipande cha
                  tamthiliya.  Hakikisha  kila  mwanafunzi  anashiriki  kikamilifu.
                  Rekebisha dosari zinazojitokeza.
           FOR ONLINE READING ONLY
             (iii)  Waelekeze wanafunzi kuandaa uwasilishaji, chagua wanafunzi
                  wachache wawasilishe kazi zao. Hakikisha kila mwanafunzi
                  anashiriki kwa kutoa mchango au kuuliza maswali. Sahihisha
                  upungufu unaojitokeza katika uwasilishaji, kisha toa mrejesho.
           Majibu


           Majibu ya shughuli ya 5.11 (a) yatategemea uelewa wa mwanafunzi.
           Katika shughuli ya hii mwanafunzi aoneshe namna alivyotumia misingi
           ya ujenzi  wa hoja  zenye mantiki  na ushawishi katika  kutathimini
           matendo ya wahusika katika kipande cha tamthiliya.

           Shughuli ya 5.11(b)

           Hatua za ufundishaji

             (i)   Waongoze wanafunzi kuchambua namna misingi ya ujenzi
                  wa hoja zenye mantiki  na ushawishi katika  kutathimini
                  matendo ya wahusika katika tamthiliya mbili teule. Hakikisha
                  kila  mwanafunzi  anashiriki  kikamilifu  katika  uchambuzi  na
                  kuchukua nukuu.

             (ii)  Kusanya na kusahihisha kazi za wanafunzi ili kuondoa upungufu
                  unaojitokeza.

           Majibu

           Majibu ya shughuli ya 5.11 (b) yatategemea uelewa wa mwanafunzi na
           tamthiliya teule atakayoichambua. Pia shughuli ya 5.11 (b) yatatokana
           na tamthiliya teule atakayoichambua mwanafunzi. Katika uchambuzi
           mwanafunzi aoneshe namna alivyotumia  misingi ya ujenzi wa hoja
           zenye mantiki na ushawishi katika kutathimini matendo ya wahusika
           katika tamthiliya mbili teule.

                 Kiongozi cha Mwalimu                                    65
                    Kidato cha Tano



                                                                            23/06/2024   17:48
     FASIHI YA KISWAHILI KIONGOZI  CHA MWALIMU KIDATO CHA TANO.indd   65    23/06/2024   17:48
     FASIHI YA KISWAHILI KIONGOZI  CHA MWALIMU KIDATO CHA TANO.indd   65
   66   67   68   69   70   71   72   73   74   75   76