Page 66 - Fasihi ya Kiswahili kwa Shule za Sekondari Kiongozi cha Mwalimu Kidato cha Tano
P. 66

Fasihi ya Kiswahili  Shule za Sekondari


             (ii)  Waongoze wanafunzi kusoma shairi lililomo  katika shughuli
                  ya 5.6 (a) iliyomo kwenye Kitabu cha Mwanafunzi, kisha
                  jibu  maswali  yanayotokana  na shairi  hilo.  Hakikisha  kila
                  mwanafunzi anasoma na kujibu maswali hayo. Rekebisha
           FOR ONLINE READING ONLY
                  dosari pale zitakapojitokeza.
             (iii)  Waelekeze wanafunzi kuandaa uwasilishaji, chagua wanafunzi
                  wachache  kujibu  swali  mojamoja  kama  alivyolichambua  na
                  kuwasilisha kwa darasa zima. Hakikisha kila mwanafunzi
                  anashiriki kwa kutoa mchango au kuuliza maswali. Sahihisha
                  upungufu unaojitokeza.

           Majibu

           Majibu ya shughuli ya 5.6 (a) yatategemea uelewa wa mwanafunzi na
           mashairi atakayoyachambua kutoka katika diwani teule. Mwanafunzi
           achambue  maana  mbalimbali  kwa kujibu  maswali  aliyopewa  kwa
           kutumia mifano kutoka katika mashairi husika.

           Shughuli ya 5.6 (b)

           Hatua za ufundishaji

             (i)   Waongoze  wanafunzi  kuchambua  mashairi  mawili  kutoka
                  katika  diwani  teule.  Hakikisha  kila  mwanafunzi  anashiriki
                  kikamilifu katika uchambuzi na kuchukua nukuu.

             (ii)  Waelekeze  wanafunzi  kukusanya kazi.  Sahihisha  kazi  hizo,
                  kisha toa mrejesho.

           Majibu

           Majibu ya shughuli ya 5.6 (b) yatategemea  uelewa wa mwanafunzi
           na mashairi atakayoyachambua  kutoka katika diwani teule. Katika
           kuchambua maana, mwanafunzi atumie mifano kutoka mashairi husika.







             60                                        Kiongozi cha Mwalimu
                                                          Kidato cha Tano



                                                                            23/06/2024   17:48
     FASIHI YA KISWAHILI KIONGOZI  CHA MWALIMU KIDATO CHA TANO.indd   60
     FASIHI YA KISWAHILI KIONGOZI  CHA MWALIMU KIDATO CHA TANO.indd   60    23/06/2024   17:48
   61   62   63   64   65   66   67   68   69   70   71