Page 70 - Fasihi ya Kiswahili kwa Shule za Sekondari Kiongozi cha Mwalimu Kidato cha Tano
P. 70

Fasihi ya Kiswahili  Shule za Sekondari



             Somo la 5: Misingi ya ujenzi wa hoja zenye mantiki na ushawishi


           Shughuli ya 5.10
           FOR ONLINE READING ONLY
           Hatua za ufundishaji

             (i)   Waongoze wanafunzi kufanya shughuli ya 5.10 iliyomo kwenye
                  Kitabu cha Mwanafunzi.

             (ii)  Waongoze  wanafunzi  kukusanya  mazungumzo  ya  makundi
                  mawili (mtoto au watoto wadogo wenye umri wa kuanza shule
                  na kiongozi yeyote wa serikali).

             (iii)  Waelekeze wanafunzi kukaa katika vikundi viwili, kila kikundi
                  kichukue aina moja ya mazungumzo na kujadili aina, maana na
                  mpangilio wake wa hoja. Hakikisha kila mwanafunzi anashiriki
                  kikamilifu. Rekebisha dosari zinazojitokeza.

             (iv)  Waongoze     wanafunzi    kuandaa     uwasilishaji   kuhusu
                  mazungumzo, kila kikundi kiwasilishe hoja zake. Hakikisha kila
                  mwanafunzi anashiriki kwa kutoa mchango au kuuliza maswali
                  ili kuendeleza mjadala. Sahihisha upungufu unaojitokeza katika
                  uwasilishaji, kisha toa mrejesho.

           Majibu

           Majibu ya shughuli 5.10 yatatokana na uelewa wa mwanafunzi. Katika
           shughuli hii, mwanafunzi ataeleza aina, maana na mpangilio wa hoja
           zinazotolewa katika mazungumzo wa kila kundi.

           Shughuli ya 5.11 (a)

           Hatua za ufundishaji

             (i)   Waongoze wanafunzi kufanya shughuli ya 5.11(a) iliyomo
                  kwenye Kitabu cha Mwanafunzi.




             64                                        Kiongozi cha Mwalimu
                                                          Kidato cha Tano



                                                                            23/06/2024   17:48
     FASIHI YA KISWAHILI KIONGOZI  CHA MWALIMU KIDATO CHA TANO.indd   64
     FASIHI YA KISWAHILI KIONGOZI  CHA MWALIMU KIDATO CHA TANO.indd   64    23/06/2024   17:48
   65   66   67   68   69   70   71   72   73   74   75