Page 72 - Fasihi ya Kiswahili kwa Shule za Sekondari Kiongozi cha Mwalimu Kidato cha Tano
P. 72
Fasihi ya Kiswahili Shule za Sekondari
Shughuli ya 5.12 (a)
Hatua za ufundishaji
(i) Waongoze wanafunzi kufanya shughuli ya 5.12 (a) iliyomo
FOR ONLINE READING ONLY
kwenye Kitabu cha Mwanafunzi ili kujenga hoja zenye mantiki
na ushawishi kuhusu ujenzi wa wahusika.
(ii) Waelekeze wanafunzi kuigiza kipande cha dailojia ya usaili, wa
kisha chambua hoja zenye mantiki na ushawishi kuhusu ujenzi
wa wahusika wake. Hakikisha kila mwanafunzi anashiriki
kikamilifu katika kuigiza na kujibu maswali kwa kutoa mifano
maridhawa. Katika uchambuzi, wanafunzi waongozwe na
maswali yaliyotolewa. Rekebisha dosari zinazojitokeza.
(iii) Waelekeze wanafunzi kuandaa uwasilishaji, kisha chagua
wanafunzi wachache wawasilishe kazi zao. Hakikisha kila
mwanafunzi anashiriki kwa kutoa mchango au kuuliza maswali.
Sahihisha upungufu unaojitokeza katika uwasilishaji, kisha toa
mrejesho.
Majibu
Majibu ya shughuli 5.12 (a) yatatokana na uelewa wa mwanafunzi.
Katika shughuli hii, mwanafunzi atajibu kwa kuongozwa na maswali
yaliyotolewa katika ujenzi wa hoja zenye ushawishi na mantiki katika
mchakato wa usaili.
Shughuli ya 5.12 (b)
Hatua za ufundishaji
(i) Waongoze wanafunzi kuandaa usaili ambao unawasilisha
hoja zenye mantiki na ushawishi katika nafasi ya kazi ambayo
mwanafunzi ataichagua. Hakikisha kila mwanafunzi anashiriki
kikamilifu katika kuandaa usaili wa kazi atakayoichagua na
kuchukua nukuu.
66 Kiongozi cha Mwalimu
Kidato cha Tano
23/06/2024 17:48
FASIHI YA KISWAHILI KIONGOZI CHA MWALIMU KIDATO CHA TANO.indd 66
FASIHI YA KISWAHILI KIONGOZI CHA MWALIMU KIDATO CHA TANO.indd 66 23/06/2024 17:48