Page 68 - Fasihi ya Kiswahili kwa Shule za Sekondari Kiongozi cha Mwalimu Kidato cha Tano
P. 68
Fasihi ya Kiswahili Shule za Sekondari
Somo la 4: Mbinu za kifasihi zinavyoathiri kupatikana kwa
maana katika kazi za kifasihi
FOR ONLINE READING ONLY
Shughuli ya 5.8 (a)
Hatua za ufundishaji
(i) Waongoze wanafunzi kufanya shughuli ya 5.8 (a) iliyomo
kwenye Kitabu cha Mwanafunzi.
(ii) Waelekeze wanafunzi kukaa katika vikundi na kujadili
shughuli ya 5.8 (a) iliyomo kwenye Kitabu cha Mwanafunzi,
kisha uliza maswali yanayowafikirisha wanafunzi. Hakikisha
kila mwanafunzi anatoa mawazo yake. Rekebisha dosari
zinazojitokeza.
(iii) Waongoze wanafunzi kuwasilisha ambapo, kila kikundi kitajibu
swali moja. Hakikisha kila mwanafunzi anashiriki kwa kutoa
mchango au kuuliza maswali ili kuendeleza mjadala. Sahihisha
upungufu unaojitokeza katika uwasilishaji, kisha toa mrejesho
wa shughuli husika.
Majibu
Majibu ya shughuli ya 5.8 (a) yatategemea uelewa wa mwanafunzi.
Katika shughuli hii, atachambua maana mbalimbali kutoka katika shairi
husika.
Shughuli ya 5.8 (b)
Hatua za ufundishaji
(i) Muongoze kila mwanafunzi kufanya shughuli 5.8 (b) kwa
kuchambua shairi moja kutoka katika diwani teule. Hakikisha
kila mwanafunzi anashiriki kikamilifu katika uchambuzi na
kuchukua nukuu.
62 Kiongozi cha Mwalimu
Kidato cha Tano
23/06/2024 17:48
FASIHI YA KISWAHILI KIONGOZI CHA MWALIMU KIDATO CHA TANO.indd 62 23/06/2024 17:48
FASIHI YA KISWAHILI KIONGOZI CHA MWALIMU KIDATO CHA TANO.indd 62