Page 65 - Fasihi ya Kiswahili kwa Shule za Sekondari Kiongozi cha Mwalimu Kidato cha Tano
P. 65
Fasihi ya Kiswahili Shule za Sekondari
Somo la 3: Maana zinazopatikana katika matini za kifasihi
Shughuli ya 5.5 (a) na (b)
FOR ONLINE READING ONLY
Hatua za ufundishaji
(i) Waongoze wanafunzi kufanya shughuli ya 5.5 (a) na (b)
zilizomo kwenye Kitabu cha Mwanafunzi.
(ii) Waelekeze wanafunzi kukaa katika vikundi vya watu wasiozidi
wanne kujadili shughuli ya 5.5 (a) iliyomo kwenye Kitabu cha
Mwanafunzi, kisha jibu maswali yaliyotolewa yanayotokana
na insha watayoijadili. Pia, kuchambua maana mbalimbali
zinazopatikana katika insha kwenye shughuli 5.5 (b). Hakikisha
kila mwanafunzi anatoa mawazo yake. Rekebisha dosari pale
zitakapojitokeza.
(iii) Waongoze wanafunzi kuandaa uwasilishaji, chagua kila
kikundi kujibu swali moja kutoka katika shughuli ya 5.5 (a)
ili kuwasilisha kwa darasa zima. Pia, chagua vikundi kadhaa
kuwasilisha maana zilizopatikana katika shughuli 5.5(b).
Hakikisha kila mwanafunzi anashiriki kwa kutoa mchango au
kuuliza maswali. Sahihisha upungufu unaojitokeza.
Majibu
Majibu ya shughuli ya 5.5 (a) na (b) yatatokana na uelewa wa
mwanafunzi. Katika shughuli hizi mwanafunzi atachambua maana
mbalimbali zinazopatikana katika insha hizo.
Shughuli ya 5.6 (a)
Hatua za ufundishaji
(i) Waongoze wanafunzi kufanya shughuli ya 5.6 (a) iliyomo
kwenye Kitabu cha Mwanafunzi.
Kiongozi cha Mwalimu 59
Kidato cha Tano
23/06/2024 17:48
FASIHI YA KISWAHILI KIONGOZI CHA MWALIMU KIDATO CHA TANO.indd 59 23/06/2024 17:48
FASIHI YA KISWAHILI KIONGOZI CHA MWALIMU KIDATO CHA TANO.indd 59