Page 62 - Fasihi ya Kiswahili kwa Shule za Sekondari Kiongozi cha Mwalimu Kidato cha Tano
P. 62

Fasihi ya Kiswahili  Shule za Sekondari


             (ii)  Waongoze  wanafunzi  kuchambua  diwani  teule  kwa kutumia
                  misingi ya ujumi. Ongoza mjadala, kisha rekebisha upungufu
                  unaojitokeza.

           Majibu
           FOR ONLINE READING ONLY
           Majibu ya shughuli ya 5.2 (c) yatategemea uelewa wa mwanafunzi na
           diwani teule  atakazozitumia mwanafunzi  katika  uchambuzi.  Katika
           uchambuzi,  mwanafunzi  azingatie  misingi  ya  ujumi  ili  kuitumia
           kuhakiki diwani teule.


             Somo la 2:  Mbinu zinazotumika kujenga ujumi katika kazi za
                        fasihi


           Shughuli ya 5.3 (a)

           Hatua za ufundishaji

             (i)   Waongoze wanafunzi kufanya shughuli ya 5.3(a) iliyomo
                  kwenye Kitabu  cha Mwanafunzi.  Ongoza mjadala  kisha
                  rekebisha upungufu unaojitokeza.

             (ii)  Waelekeze  wanafunzi  kukaa  katika  jozi  na  kujadili  shughuli
                  ya 5.3 (a) iliyomo kwenye Kitabu cha Mwanafunzi, kisha
                  uliza  maswali  yanayowafikirisha  wanafunzi.  Hakikisha  kila
                  mwanafunzi anatoa mawazo yake. Rekebisha dosari pale
                  zinapojitokeza.

             (iii)  Waongoze  wanafunzi  kuandaa  uwasilishaji,  chagua  vikundi
                  vichache ili kuwakilisha vingine. Hakikisha kila mwanafunzi
                  anashiriki kwa kutoa mchango au kuuliza maswali. Sahihisha
                  upungufu unaojitokeza, kisha toa mrejesho wa shughuli husika.









             56                                        Kiongozi cha Mwalimu
                                                          Kidato cha Tano



                                                                            23/06/2024   17:48
     FASIHI YA KISWAHILI KIONGOZI  CHA MWALIMU KIDATO CHA TANO.indd   56    23/06/2024   17:48
     FASIHI YA KISWAHILI KIONGOZI  CHA MWALIMU KIDATO CHA TANO.indd   56
   57   58   59   60   61   62   63   64   65   66   67