Page 59 - Fasihi ya Kiswahili kwa Shule za Sekondari Kiongozi cha Mwalimu Kidato cha Tano
P. 59
Fasihi ya Kiswahili Shule za Sekondari
Sura ya
Tano Ujumi katika kazi za fasihi
FOR ONLINE READING ONLY
Utangulizi
Katika sura hii, mwanafunzi atajifunza kuhusu ujumi unavyojitokeza
katika fasihi simulizi na fasihi andishi. Pia, atajifunza kueleza na
kuchambua mbinu zilizotumika kiujumi katika majigambo, mashairi
na tamthiliya teule. Aidha, atajifunza jinsi mbinu za kifasihi
zinavyodhihirika katika kujenga maana katika insha za kifasihi,
mashairi na tamthiliya. Kadhalika, atajifunza namna ya kutumia
fasihi katika kujenga hoja zenye mantiki na ushawishi. Mwalimu
utapata mbinu zitakazokuwezesha katika ujenzi wa umahiri huu kwa
mwanafunzi.
Shughuli za kutendwa na mwanafunzi
(a) Kueleza vigezo vya ujenzi wa ujumi katika kazi za kifasihi;
(b) Kufafanua mbinu zilizotumika kujenga ujumi katika kazi za
kifasihi;
(c) Kueleza maana zinazopatikana katika matini za fasihi;
(d) Kuchambua mbinu za kifasihi zinavyoathiri kupatikana kwa
maana katika kazi za kifasihi;
(e) Misingi ya ujenzi wa hoja zenye mantiki na ushawishi;
Kiongozi cha Mwalimu 53
Kidato cha Tano
23/06/2024 17:48
FASIHI YA KISWAHILI KIONGOZI CHA MWALIMU KIDATO CHA TANO.indd 53 23/06/2024 17:48
FASIHI YA KISWAHILI KIONGOZI CHA MWALIMU KIDATO CHA TANO.indd 53