Page 54 - Fasihi ya Kiswahili kwa Shule za Sekondari Kiongozi cha Mwalimu Kidato cha Tano
P. 54

Fasihi ya Kiswahili  Shule za Sekondari


           Shughuli ya 4.13(b)
           Hatua za ufundishaji

             (i)   Unaweza  kutumia  mbinu  ya changanya  kete  kuwaongoza
           FOR ONLINE READING ONLY
                  wanafunzi kuhusisha mitazamo ya jamii na mawazo yaliyomo
                  katika mashairi mbalimbali yaliyomo  kwenye diwani teule.

             (ii)  Waongoze wanafunzi kukaa katika vikundi kuchambua shughuli
                  ya 4.13 (b) iliyomo  kwenye Kitabu  cha  Mwanafunzi,  kisha
                  wakusanye kazi zao. Sahihisha na toa mrejesho kwa wanafunzi.

           Majibu

           Majibu ya shughuli ya 4.13 (b) yatatokana na uelewa wa mwanafunzi.
           Katika shughuli hii, mwanafunzi atachambua na kuhusianisha matendo
           ya jamii na mitazamo iliyomo kwenye mashairi mawili ya diwani teule.


           Shughuli ya 4.14(a)

           Hatua za ufundishaji
             (i)   Waongoze wanafunzi kusoma kipande cha tamthiliya kilichomo
                  katika shughuli 4.14(a) kwenye Kitabu cha Mwanafunzi, kisha
                  kukaa  katika  vikundi  ili  kuhusisha mitazamo  ya jamii  na
                  mawazo yaliyomo kwenye kipande cha tamthiliya.

             (ii)  Waongoze wanafunzi kuwasilisha darasani kazi walizozifanya
                  katika vikundi vyao kwa majadiliano zaidi huku ukirekebisha
                  upungufu unaojitokeza wakati wa uwasilishaji.

           Majibu

           Majibu ya shughuli ya 4.14 (a) yatatokana na uelewa wa mwanafunzi.
           Katika shughuli hii, mwanafunzi atachambua na kuhusianisha mitazamo
           na matendo ya jamii kwa kujibu maswali yaliyotolewa.







             48                                        Kiongozi cha Mwalimu
                                                          Kidato cha Tano



                                                                            23/06/2024   17:48
     FASIHI YA KISWAHILI KIONGOZI  CHA MWALIMU KIDATO CHA TANO.indd   48    23/06/2024   17:48
     FASIHI YA KISWAHILI KIONGOZI  CHA MWALIMU KIDATO CHA TANO.indd   48
   49   50   51   52   53   54   55   56   57   58   59