Page 49 - Fasihi ya Kiswahili kwa Shule za Sekondari Kiongozi cha Mwalimu Kidato cha Tano
P. 49
Fasihi ya Kiswahili Shule za Sekondari
Somo la 3: Mitazamo iliyomo katika bongo fleva, mashairi na
tamthiliya
FOR ONLINE READING ONLY
Shughuli ya 4.9 (a)
Hatua za ufundishaji
(i) Waongoze wanafunzi kwa njia ya maswali na majibu kubainisha
mitazamo iliyomo katika jamii.
(ii) Waongoze wanafunzi kutumia vyanzo vya mtandaoni au
vinginevyo kusikiliza au kutazama wimbo wa bongo fleva
unaosawiri athari za starehe kisha kukaa katika vikundi
visivyozidi wanafunzi watano kujadiliana kuhusu shughuli ya
4.9(a) iliyomo kwenye Kitabu cha Mwanafunzi.
(iii) Waongoze wanafunzi kuwasilisha, unaweza kuchagua baadhi
ya vikundi kuwasilisha kwa niaba ya vikundi vingine. Sisitiza
ushiriki wa kila mwanafunzi kwa kuchangia mawazo wakati
wa uwasilishaji.
(iv) Rekebisha upungufu unaojitokeza wakati wa uwasilishaji ili
kuleta uelewa wa pamoja.
Majibu
Majibu ya shughuli ya 4.9 (a) yatatokana na uelewa wa mwanafunzi.
Katika shughuli hii, mwanafunzi atachambua mitazamo kwa kuongozwa
na maswali yaliyomo katika Kitabu cha Mwanafunzi.
Shughuli ya 4.9(b)
Hatua za ufundishaji
(i) Waelekeze wanafunzi kupakua na kusikiliza au kutazama
nyimbo mbili za bongo fleva, kisha kuchambua mitazamo
Kiongozi cha Mwalimu 43
Kidato cha Tano
23/06/2024 17:48
FASIHI YA KISWAHILI KIONGOZI CHA MWALIMU KIDATO CHA TANO.indd 43 23/06/2024 17:48
FASIHI YA KISWAHILI KIONGOZI CHA MWALIMU KIDATO CHA TANO.indd 43