Page 46 - Fasihi ya Kiswahili kwa Shule za Sekondari Kiongozi cha Mwalimu Kidato cha Tano
P. 46

Fasihi ya Kiswahili  Shule za Sekondari


           Majibu
           Majibu ya shughuli ya 4.6 (a) yatatokana na uelewa wa mwanafunzi.
           Katika shughuli hizi, mwanafunzi atachambua maadili  kwa
           kuyalinganisha na masuala ya kiimani yaliyomo katika kazi hizo. Ili
           FOR ONLINE READING ONLY
           kufanya shughuli hizi kwa ufanisi, mwanafunzi anapaswa kuyafahamu
           vizuri maadili na imani za jamii yake.

           Shughuli ya 4.6 (b)

           Hatua za ufundishaji

             (i)   Waongoze wanafunzi kufanya shughuli ya 4.6 (a) iliyomo
                  kwenye Kitabu cha Mwanafunzi.

             (ii)  Waelekeze  wanafunzi  kukaa  katika  vikundi  ili  kupakua  na
                  kusikiliza  nyimbo  za  bongo  fleva,  kisha  kuchambua  maadili
                  yaliyomo katika nyimbo hizo.
             (iii)  Teua wanafunzi wachache, kisha waongoze kuwasilisha kwa
                  niaba  ya  wengine.  Hakikisha  kila  mwanafunzi  anashiriki
                  kikamilifu  wakati wa uwasilishaji. Rekebisha upungufu
                  unaojitokeza wakati wa uwasilishaji.

           Shughuli ya 4.7(a)

           Hatua za ufundishaji

             (i)   Waongoze wanafunzi kukaa katika vikundi kughani au kusoma
                  shairi lililomo katika shughuli ya 4.7(a) iliyomo kwenye Kitabu
                  cha Mwanafunzi.

             (ii)  Waongoze wanafunzi kujadiliana katika jozi, shughuli ya 4.7(a)
                  iliyomo kwenye Kitabu cha Mwanafunzi, kisha teua baadhi ya
                  jozi  ziwasilishe  darasani.  Rekebisha  upungufu unaojitokeza
                  wakati wa uwasilishaji.






             40                                        Kiongozi cha Mwalimu
                                                          Kidato cha Tano



                                                                            23/06/2024   17:48
     FASIHI YA KISWAHILI KIONGOZI  CHA MWALIMU KIDATO CHA TANO.indd   40    23/06/2024   17:48
     FASIHI YA KISWAHILI KIONGOZI  CHA MWALIMU KIDATO CHA TANO.indd   40
   41   42   43   44   45   46   47   48   49   50   51