Page 41 - Fasihi ya Kiswahili kwa Shule za Sekondari Kiongozi cha Mwalimu Kidato cha Tano
P. 41

Fasihi ya Kiswahili  Shule za Sekondari


           Shughuli ya 4.2 (a)
           Hatua za ufundishaji

             (i)   Waongoze wanafunzi kutumia vyanzo vya mkondoni kupakua
           FOR ONLINE READING ONLY
                  na  kusikiliza  wimbo  wowote  wa  bongo  fleva  unaosawiri
                  umuhimu wa wazazi, kisha kila mwanafunzi  ajibu maswali
                  yaliyomo kwenye Kitabu cha Mwanafunzi.

             (ii)  Waongoze wanafunzi kuandaa uwasilishaji. Chagua baadhi ya
                  wanafunzi wawasilishe kazi zao darasani kwa majadiliano huku
                  ukirekebisha upungufu unaojitokeza wakati wa uwasilishaji.
             (iii)  Waongoze wanafunzi kuhitimisha kwa kutoa maelezo ya jumla
                  kuhusu shughuli husika.

           Majibu

           Majibu ya shughuli ya 4.2 (a) yatatokana  na uelewa wa mwanafunzi.
           Katika shughuli hii, mwanafunzi atachambua maadili kwa kuongozwa
           na maswali yaliyotolewa. Mwanafunzi atumie mifano kutoka kwenye
           wimbo husika na kuhusianisha hoja zake na maisha halisi.

           Shughuli ya 4.2(b)

           Hatua za ufundishaji

             (i)   Waongoze wanafunzi kutumia vifaa vya TEHAMA kupakua na
                  kusikiliza nyimbo za bongo fleva.

             (ii)  Waongoze wanafunzi kukaa katika jozi na kila jozi ichambue
                  maadili ya wimbo mmojawapo kati ya walizozisiliza.
             (iii)  Waongoze wanafunzi kukusanya, sahihisha na toa mrejesho wa
                  kazi zao.









                 Kiongozi cha Mwalimu                                    35
                    Kidato cha Tano



                                                                            23/06/2024   17:48
     FASIHI YA KISWAHILI KIONGOZI  CHA MWALIMU KIDATO CHA TANO.indd   35    23/06/2024   17:48
     FASIHI YA KISWAHILI KIONGOZI  CHA MWALIMU KIDATO CHA TANO.indd   35
   36   37   38   39   40   41   42   43   44   45   46