Page 36 - Fasihi ya Kiswahili kwa Shule za Sekondari Kiongozi cha Mwalimu Kidato cha Tano
P. 36
Fasihi ya Kiswahili Shule za Sekondari
uwasilishaji.
(ii) Waongoze wanafunzi kuhusianisha misingi ya nadharia ya
uumundo wakati wa uchambuzi wa shairi hilo.
FOR ONLINE READING ONLY
(iii) Rekebisha upungufu unaojitokeza wakati wa uwasilishaji.
Majibu
Majibu ya shughuli ya 3.14 yatatokana na uelewa wa mwanafunzi.
Katika shughuli hii, mwanafunzi ahakiki shairi kwa kutumia nadharia
ya umuundo. Hakikisha mwanafunzi anatumia misingi ya nadharia
husika na mifano kutoka katika kazi teule ya kifasihi.
Shughuli ya 3.15 (a)
Hatua za ufundishaji
(i) Unda jozi za wanafunzi, kisha waongoze kughani au kusoma
shairi lililomo katika shughuli ya 3.15 (a) kwenye Kitabu
cha Mwanafunzi kwa kupokezana, huku wakiandika nukuu
muhimu.
(ii) Waongoze wanafunzi kuchambua shairi kwa kutumia maswali
ya mwongozo yaliyowekwa baada ya shairi hilo.
(iii) Kwa njia ya maswali na majibu, waongoze wanafunzi
kuwasilisha uchambuzi walioufanya kwa kuhusanisha na
misingi ya nadharia ya umuundo.
Majibu
Majibu ya shughuli ya 3.15 (a) yatatokana na uelewa wa mwanafunzi.
Katika shughuli 3.15 (a) iliyomo kwenye Kitabu cha Mwanafunzi,
hakikisha mwanafunzi anahakiki mashairi mawili kutoka katika diwani
teule kwa kutumia nadharia ya umuundo.
30 Kiongozi cha Mwalimu
Kidato cha Tano
23/06/2024 17:48
FASIHI YA KISWAHILI KIONGOZI CHA MWALIMU KIDATO CHA TANO.indd 30 23/06/2024 17:48
FASIHI YA KISWAHILI KIONGOZI CHA MWALIMU KIDATO CHA TANO.indd 30