Page 35 - Fasihi ya Kiswahili kwa Shule za Sekondari Kiongozi cha Mwalimu Kidato cha Tano
P. 35

Fasihi ya Kiswahili  Shule za Sekondari



             Somo la 6:  Kuhahiki maigizo  mashairi  na tamthiliya  kwa
                        kutumia nadharia za kifashi


           FOR ONLINE READING ONLY
           Shughuli ya 3.13

           Hatua za ufundishaji
             (i)   Waongoze  wanafunzi  kutazama  au kusikiliza  maigizo kwa
                  kutumia vifaa vya TEHAMA, mwanafunzi anaweza kusikiliza
                  au kutazama akiwa nyumbani au shuleni kulingana na mazingira
                  yake huku akinukuu dondoo muhimu kuhusiana na maswali ya
                  mwongozo yaliyomo katika shughuli ya 3.13(a) na (b) i - v.

             (ii)  Waelekeze wanafunzi kukaa katika vikundi na kujadili shughuli
                  ya 3.13(a) na (b)  zilizopo kwenye Kitabu cha Mwanafunzi,
                  kisha kufanya uwasilishaji.  Hakikisha  kila  mwanafunzi
                  anashiriki katika uwasilishaji.

             (iii)  Rekebisha upungufu unaojitokeza wakati wa uwasilishaji.

           Majibu

           Majibu  ya  shughuli  ya  3.13  yatatokana  na  uelewa  wa  mwanafunzi.
           Katika shughuli 3.13(a) mwanafunzi ahakiki igizo kwa kutumia nadharia
           ya uhalisia. Katika shughuli 3.13(b), mwanafunzi atumie nadharia ya
           mwitiko wa msomaji katika kuhakiki maigizo matatu aliyoyatazama
           au kuyasikiliza. Hakikisha mwanafunzi anatumia misingi ya nadharia
           husika kwa kuongozwa na maswali i – v yaliyotolewa.

           Shughuli ya 3.14

           Hatua za ufundishaji

             (i)   Waongoze wanafunzi kusoma shairi lililomo katika shughuli ya
                  3.14 iliyomo kwenye Kitabu cha Mwanafunzi huku wakinukuu
                  dondoo muhimu  wakati  wa uchambuzi,  kisha kufanya
                  uwasilishaji.  Hakikisha  kila  mwanafunzi  anashiriki katika

                 Kiongozi cha Mwalimu                                    29
                    Kidato cha Tano



                                                                            23/06/2024   17:48
     FASIHI YA KISWAHILI KIONGOZI  CHA MWALIMU KIDATO CHA TANO.indd   29    23/06/2024   17:48
     FASIHI YA KISWAHILI KIONGOZI  CHA MWALIMU KIDATO CHA TANO.indd   29
   30   31   32   33   34   35   36   37   38   39   40