Page 40 - Fasihi ya Kiswahili kwa Shule za Sekondari Kiongozi cha Mwalimu Kidato cha Tano
P. 40
Fasihi ya Kiswahili Shule za Sekondari
(d) Kuhusianisha mitazamo iliyomo katika nyimbo za bongo
fleva, mashairi na tamthiliya na matendo ya jamii ; na
(e) Kujadili namna athari za kiimani na kimitazamo katika bongo
fleva, mashairi na tamthiliya zinavyojidhihirisha katika jamii.
FOR ONLINE READING ONLY
Mahitaji: Matini na makala za kifasihi, magazeti, nyimbo za bongo
fleva, mashairi na tamthiliya zilizorekodiwa, vitabu teule, na
chati ya alama za LAT.
Somo la 1: Maadili katika nyimbo za bongo fleva, mashairi na
tamthiliya
Shughuli ya 4.1
Hatua za ufundishaji
(i) Waongoze wanafunzi kutumia vifaa vya TEHAMA kupakua na
kusikiliza au kutazama wimbo mmoja ambao unaona kuwa una
maadili na mwingine ambao hauna maadili kisha kukaa katika
jozi na kujadili shughuli ya 4.1 iliyomo kwenye Kitabu cha
Mwanafunzi.
(ii) Waongoze wanafunzi kuandaa uwasilishaji kwa kuchagua
wanafunzi wachache kuwasilisha kazi zao na wengine
washiriki kwa kuuliza maswali na kuchangia hoja. Rekebisha
upungufu unaojitokeza wakati wa uwasilishaji ili kuleta uelewa
wa pamoja.
Majibu
Majibu ya shughuli ya 4.1 yatatokana na uelewa wa mwanafunzi.
Katika shughuli hii, mwanafunzi atachambua sababu za wimbo huo
mmoja kuwa na mwingine kukosa maadili.
34 Kiongozi cha Mwalimu
Kidato cha Tano
23/06/2024 17:48
FASIHI YA KISWAHILI KIONGOZI CHA MWALIMU KIDATO CHA TANO.indd 34 23/06/2024 17:48
FASIHI YA KISWAHILI KIONGOZI CHA MWALIMU KIDATO CHA TANO.indd 34