Page 44 - Fasihi ya Kiswahili kwa Shule za Sekondari Kiongozi cha Mwalimu Kidato cha Tano
P. 44
Fasihi ya Kiswahili Shule za Sekondari
(ii) Waelekeze wanafunzi kukaa katika kikundi cha wanafunzi
wasiozidi wanne, kisha wachambue maadili yaliyomo katika
tamthiliya mbili teule.
(iii) Waongoze wanafunzi kuwasilisha maadili yaliyomo katika
FOR ONLINE READING ONLY
tamthiliya teule, kisha chagua vikundi vichache ili viwasilishe
kazi zao. Hakikisha kila mwanafunzi anashiriki kikamilifu
kisha kusanya kazi za wanafunzi.
(iv) Sahihisha kazi ya kila mwanafunzi ili kuondoa dosari
zinazojitokeza na toa mrejesho kwa wanafunzi wote.
Majibu
Majibu ya shughuli ya 4.4 (b) yatatokana na uelewa wa mwanafunzi.
Katika shughuli hii, mwanafunzi atachambua maadili yaliyomo katika
tamthiliya teule.
Shughuli ya 4.4(c)
Hatua za ufundishaji
(i) Waongoze wanafunzi kufanya shughuli ya 4.4 (c) iliyomo
kwenye Kitabu cha Mwanafunzi.
(ii) Waelekeze wanafunzi kukaa katika vikundi ili kupakua na
kusikiliza tamthiliya mbili kisha kuchambua maadili yaliyomo
katika tamthiliya hizo mbili zinazorushwa katika vituo vya
runinga.
(iii) Waongoze wanafunzi kuwasilisha kwa kuchagua wanafunzi
wachache kuwasilisha kwa niaba ya wengine. Hakikisha kila
mwanafunzi anashiriki kikamilifu wakati wa uwasilishaji.
(iv) Rekebisha upungufu unaojitokeza wakati wa uwasilishaji.
Majibu
Majibu ya shughuli ya 4.4 (c) yatatokana na uelewa wa mwanafunzi.
Katika shughuli hii, mwanafunzi atatumia mifano kuchambua maadili
yaliyomo katika tamthiliya hizo mbili.
38 Kiongozi cha Mwalimu
Kidato cha Tano
23/06/2024 17:48
FASIHI YA KISWAHILI KIONGOZI CHA MWALIMU KIDATO CHA TANO.indd 38
FASIHI YA KISWAHILI KIONGOZI CHA MWALIMU KIDATO CHA TANO.indd 38 23/06/2024 17:48