Page 45 - Fasihi ya Kiswahili kwa Shule za Sekondari Kiongozi cha Mwalimu Kidato cha Tano
P. 45

Fasihi ya Kiswahili  Shule za Sekondari



             Somo la 2:  Ulinganisho wa maadili  yaliyomo  katika kazi za
                        fasihi na imani za jamii


           Shughuli ya 4.5
           FOR ONLINE READING ONLY
           Hatua za ufundishaji
             (i)   Kwa njia ya bungua bongo, waongoze wanafunzi kubainisha
                  imani zilizomo katika jamii.

             (ii)  Waongoze wanafunzi kutumia vyanzo mbalimbali kusoma kazi
                  nne za ushairi na nne za tamthiliya kisha kukaa katika vikundi
                  ili  kuchambua  masuala  ya  kiimani  yaliyomo  katika  kazi
                  hizo. Hakikisha kila mwanafunzi anashiriki kikamilifu katika
                  majadiliano na kutoa mawazo yake wakati wa uwasilishaji.

             (iii)  Hitimisha kwa kutoa maelezo ya jumla kuhusu shughuli ya 4.5
                  ili kuleta uelewa wa pamoja.
           Majibu

           Majibu ya shughuli ya 4.5 yatatokana na uelewa wa mwanafunzi. Katika
           shughuli  hii,  mwanafunzi  atachambua  masuala  ya  kiimani  yaliyomo
           katika kazi hizo kulingana na jamii yake.

           Shughuli ya 4.6 (a)

           Hatua za ufundishaji

             (i)   Waongoze wanafunzi kutumia vyanzo mbalimbali kupakua na
                  kusikiliza nyimbo zinazohusiana na shughuli ya 4.6 (a) iliyomo
                  kwenye Kitabu cha Mwanafunzi.

             (ii)  Waelekeze wanafunzi kukaa katika jozi na kufanya shughuli
                  ya  4.6 (a)  iliyomo  kwenye  Kitabu  cha  Mwanafunzi  kisha
                  wakusanye kazi zao.

             (iii)  Sahihisha na toa mrejesho ili kuleta uelewa wa pamoja.

                 Kiongozi cha Mwalimu                                    39
                    Kidato cha Tano



                                                                            23/06/2024   17:48
     FASIHI YA KISWAHILI KIONGOZI  CHA MWALIMU KIDATO CHA TANO.indd   39    23/06/2024   17:48
     FASIHI YA KISWAHILI KIONGOZI  CHA MWALIMU KIDATO CHA TANO.indd   39
   40   41   42   43   44   45   46   47   48   49   50