Page 47 - Fasihi ya Kiswahili kwa Shule za Sekondari Kiongozi cha Mwalimu Kidato cha Tano
P. 47

Fasihi ya Kiswahili  Shule za Sekondari


             (iii)  Hitimisha kwa kutoa maelezo ya jumla kuhusiana na shughuli
                  ya 4.7(a) ili kuleta uelewa wa pamoja.

           Majibu

           FOR ONLINE READING ONLY
           Majibu ya shughuli ya 4.7 (a) yatatokana na uelewa wa mwanafunzi.
           Katika  shughuli hii, mwanafunzi  alinganishe  maadili  na masuala  ya
           kiimani yaliyomo katika kazi hizo.

           Shughuli ya 4.7(b)

           Hatua za ufundishaji

             (i)   Waongoze wanafunzi kufanya shughuli ya 4.7 (b) iliyomo
                  kwenye Kitabu cha Mwanafunzi.

             (ii)  Waongoze  wanafunzi  kusoma diwani mbili  teule, kisha
                  wachambue  maadili  yaliyomo.  Baadaye  waandae  matini  ya
                  uchambuzi na kuikusanya kwa ajili ya maboresho.

             (iii)  Sahihisha kazi ya kila mwanafunzi ili kuondoa dosari
                  zinazojitokeza na toa mrejesho kwa wanafunzi wote.

           Majibu

           Majibu ya shughuli ya 4.7 (b) yatatokana na uelewa wa mwanafunzi.
           Katika shughuli hii, mwanafunzi atachambua na kuhusianisha maadili
           yaliyomo na imani za jamii katika mashairi mawili ya diwani teule.

           Shughuli ya 4.8(a)

           Hatua za ufundishaji

             (i)   Waongoze wanafunzi kusoma matini fupi ya tamthiliya iliyomo
                  kwenye shughuli ya 4.8(a) katika Kitabu cha Mwanafunzi, kisha
                  kujadiliana katika vikundi kwa kujibu maswali yaliyotolewa.

             (ii)  Waelekeze  wanafunzi  kuandaa  uwasilishaji,  kisha chagua
                  wanafunzi  wachache  wawasilishe  kazi  zao  kwa  niaba  ya


                 Kiongozi cha Mwalimu                                    41
                    Kidato cha Tano



                                                                            23/06/2024   17:48
     FASIHI YA KISWAHILI KIONGOZI  CHA MWALIMU KIDATO CHA TANO.indd   41    23/06/2024   17:48
     FASIHI YA KISWAHILI KIONGOZI  CHA MWALIMU KIDATO CHA TANO.indd   41
   42   43   44   45   46   47   48   49   50   51   52