Page 48 - Fasihi ya Kiswahili kwa Shule za Sekondari Kiongozi cha Mwalimu Kidato cha Tano
P. 48

Fasihi ya Kiswahili  Shule za Sekondari


                  wenzao huku wengine wakichangia hoja na kuuliza maswali ili
                  kuendeleza majadiliano zaidi. Rekebisha upungufu unaojitokeza
                  wakati wa uwasilishaji.

             (iii)  Hitimisha kwa kutoa maelezo ya jumla kuhusiana na shughuli
           FOR ONLINE READING ONLY
                  husika.

           Majibu

           Majibu ya shughuli ya 4.8 (a) yatatokana na uelewa wa mwanafunzi.
           Katika shughuli hii, mwanafunzi atatakiwa  kulinganisha maadili  na
           masuala ya kiimani yaliyomo katika kipande hicho cha tamthiliya kwa
           kujibu maswali i - v.

           Shughuli ya 4.8(b)

           Hatua za ufundishaji

             (i)   Waongoze wanafunzi kufanya shughuli ya 4.8 (b) iliyomo
                  kwenye Kitabu cha Mwanafunzi.

             (ii)  Waongoze wanafunzi kuchambua maadili  yaliyomo katika
                  tamthiliya teule mbili, kisha waandae matini ya uchambuzi na
                  kuikusanya kwa ajili ya maboresho.

             (iii)  Sahihisha kazi ya kila mwanafunzi ili kuondoa dosari
                  zinazojitokeza na toa mrejesho kwa wanafunzi wote.

           Majibu

           Majibu ya shughuli ya 4.8 (b) yatatokana na uelewa wa mwanafunzi.
           Katika shughuli hii, mwanafunzi atachambua na kuhusianisha maadili
           yaliyomo na imani za jamii katika tamthiliya teule mbili.











             42                                        Kiongozi cha Mwalimu
                                                          Kidato cha Tano



                                                                            23/06/2024   17:48
     FASIHI YA KISWAHILI KIONGOZI  CHA MWALIMU KIDATO CHA TANO.indd   42
     FASIHI YA KISWAHILI KIONGOZI  CHA MWALIMU KIDATO CHA TANO.indd   42    23/06/2024   17:48
   43   44   45   46   47   48   49   50   51   52   53