Page 43 - Fasihi ya Kiswahili kwa Shule za Sekondari Kiongozi cha Mwalimu Kidato cha Tano
P. 43
Fasihi ya Kiswahili Shule za Sekondari
(iii) Waongoze wanafunzi kuwasilisha maadili yaliyomo katika
mashairi, chagua vikundi vichache ili uwasilishe kazi zao,
hakikisha kila mwanafunzi anashiriki kikamilifu kisha kusanya
kazi za wanafunzi.
FOR ONLINE READING ONLY
(iv) Sahihisha kazi ya kila mwanafunzi ili kuondoa dosari
zinazojitokeza na toa mrejesho kwa wanafunzi wote.
Majibu
Majibu ya shughuli ya 4.3 (b) yatatokana na uelewa wa mwanafunzi.
Katika shughuli hii, mwanafunzi atachambua maadili yaliyomo katika
mashairi kutoka katika diwani teule.
Shughuli ya 4.4(a)
Hatua za ufundishaji
(i) Waongoze wanafunzi kusoma matini fupi ya tamthiliya iliyomo
katika shughuli ya 4.4 (a) katika Kitabu cha Mwanafunzi.
(ii) Kwa njia ya maswali na majibu, waongoze wanafunzi kujibu
maswali yaliyopo baada ya matini fupi ya tamthiliya.
(iii) Waelekeze wanafunzi kuchambua maadili kisha kukusanya
kazi zao. Sahihisha na toa mrejesho wa shughuli hiyo kwa
wanafunzi wote.
Majibu
Majibu ya shughuli ya 4.4 (a) yatatokana na uelewa wa mwanafunzi.
Katika shughuli hii, mwanafunzi atachambua maadili kwa kuongozwa
na maswali yaliyomo katika Kitabu cha Mwanafunzi.
Shughuli ya 4.4(b)
Hatua za ufundishaji
(i) Waongoze wanafunzi kufanya shughuli ya 4.4 (b) iliyomo
kwenye Kitabu cha Mwanafunzi.
Kiongozi cha Mwalimu 37
Kidato cha Tano
23/06/2024 17:48
FASIHI YA KISWAHILI KIONGOZI CHA MWALIMU KIDATO CHA TANO.indd 37 23/06/2024 17:48
FASIHI YA KISWAHILI KIONGOZI CHA MWALIMU KIDATO CHA TANO.indd 37